13 May 2012

Safari Bado Ndefu.........Muziki Wa Injili Umekuwa Wadunia?? a.k.a Gospesecular?

Kila Jumapili ambayo Mungu atakuwa anatujalia uzima tutakuwa tunatazama mambo ambayo yanatupa mawazo ya kila iitwapo leo na kuona kabisa Safari Bado Ndefu. Kumekuwa na mambo mengi katika Wana Wa Mungu ambayo haya tukiyatazama kwa kina ni kuona "Bado Safari Ndefu" Kuelekea tunakopaswa kuelekea. Kumekuwa na Controversial za kutosha zinazotokana na mitazamo ya Watu.
                       The Glorious Wakiwa Jukwaani Wakati Wa Gospel Music Awards.

Nia ya Segment hii kwenye Blog ni Kuibua Mawazo ama mitazamo ya watu ambao watawasilisha Mawazo yao Mbadala katika kuona mambo yanavyokwenda ndivyo yanavyopaswa nia kubwa ni Kupunguza Umbali wa Safari kwa Kuleta mawazo mapya ndani ya Jamii yetu Kupitia Blog hii. 



Hakuna shaka kwamba sasa Tanzania Muziki wa Injili unakua na kuongezeka kwa kiwango cha kushangaza kama sio cha kazi kubwa. Kumekuwa na matamasha kila iitwapo leo, kumekuwa na events za uimbaji zenye majina tofauti tofauti, huku amplified Praise and Worship, Huku Aflewo, Huku Maximum Praise and Worship, Huku Next Level,  Huku Gospel Music Awards, Huku Tamasha la Pasaka, huku Gospel Star Search na majina kadha wa kadha. 
                              Samuel Rodin Akiwa kwenye Event Ya Next Level

Kwenye Televisions na Radio vipindi vya Gospel Tracks na kadha wa kadha mpaka kwenye radio za Secular wamekuwa na vipindi maalum vya muziki wa Injili.

Kila mtu amekuwa na jitihada binafsi za kutaka kukuza Muziki huu wa unaoitwa Muziki wa Wa Injili.
                             Kyala Dee Mwanamuziki Wa Kitanzania Anayefanya Muziki Ughaibuni

Katika kasi hii wameibuka waimbaji wengi sana katika tasnia hii ya unaoitwa Muziki Wa Injili. Wanamuziki hawa kutokana na utashi wao wamekuwa wakiandaa albam zao either kwa kiwango cha chini ama kueshindwa kuendelea ku hit kwenye gospel music kwa sababu moja ama nyingine kutokana na matokeo wanayoyapata kutoka kwa wasambazaji wa Kazi za Muziki wa Injili.
    Christina Shusho Mshindi Wa Tuzo za "Grooves Awards" 2011-2012 Nchini Kenya.

Ukienda kwenye Maharusi, Kitchen Parties, Misiba kila mahali Muziki wa Injili umekuwa ukitumika kama ndicho kuburudisha muafaka wa tafrija hizo katika nchi yetu ya Tanzania.
Kutokana na Kukua kwa "Gospel Music Industry" na Sio Gospel Music Ministry kumepelekea Muziki wa Injili Kuibua Maswali mengi kama Kweli Muziki huu unapaswa kuendelea Kuitwa Muziki Wa Injili.
Emmanuel na Flora Mbasha Wanamuziki ambao Kwa Kipindi hiki wako Marekani hapo walipokuwa "Voice Of America".


Maneno yanayoimbwa kwenye nyimbo hizo yameendeleea kuleta maswali kama ni Muziki wa Injili, Uvaaji wa Wanamuziki Umeendelea Kuwa ni Utata katika Majukwaa na kuondoa hadhi ya Injili, Uchezaji katika Majukwaa umeibua mijadala mizito na kukosa mwelekeo kwa kutaka kufahamu bado kama kuna hadhi ya Kuwa na Muziki wa Injili Tanzania.


Kumekuwa na mijadala ya kila siku kuwa Muziki wa Injili Tanzania Umevamiwa na Watu wasio wa Injili. Kuna Maswali yameibuliwa ambayo yanatafuta majibu katika Jamii yetu.

Gee and Seth Wanaofanya Muziki Wa Hip Pop Walipokuwa ndani ya Event Ya Riot.


1. Muziki wa Injili ni Upi, how can we clearly define Gospel Music, kwa maana vigezo gani vinaufanya wimbo fulani kutokuwa wa injili na fulani ni wimbo wa injili.


2. Unaitwa Wimbo wa Injili Sababu unaimbwa wimbo na Mkristo ama mtu yeyote anaweza kuimba kwa kuimba maneno ya Mungu "Kikristo".


3. Kwa Watu Wasiomjua Mungu kwenye Maisha yao kama Waandaaji wa Matamasha, Waandaaji wa Tuzo za Muziki wa Injili, Wasambazaji wa Kazi za Muziki wa Injili, Waandaaji Wa  Kazi za Muziki wa Injili, Mameneja wa Kazi za Injili na Watangazaji wa Radio na TV ni sahihi kwao "Ku-Promote" muziki wa Injili???


4. Je Ni sahihi Mwanamuzi wa Injili kutaja "dau" lake na kulipwa kabla ya huduma??
       Addo November Rais Wa Shirikisho la Wanamuziki Wa Injili Tanzania.


5. Ni sahihi Kwa Wanamuziki wa Injili Kushirika katika Matamasha yaliyoandaliwa na Wadunia??Kushiriki tuzo zisizo za Kimungu mfn. Kills Music Awards e.tc.


6. Ni Sahihi kumuita Mwanamuziki wa Injili Star??"Nyota Wa Muziki Wa Injili.


Kwa Wiki Kadha zijazo nitakuwa ninajibu maswali haya kadha wa Kadha Kwenye Bloga huku nikipikea mawazo.


Kama una maoni kuhusiana na maswali hapo juu tuma kwenda 


1. Email Address....samuelsasali@gmail.com
2. Mobile Number.  0713 494110
3. Facebook Account.. Samuel Sasali

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...