27 February 2012

KUMBE BOB MARLEY ALIOKOKA HII NI YENYEWE.


Nini maana ya Rastafari? na wanaamini nini?

Kuna watu wanampenda Bob Marley ama wanasema wanafuata nyayo au kuiga mfano wake, lakini ziko habari kwamba Bob Marley kabla hajafa alimpokea Bwana Yesu na kubatizwa kuwa muumini wa Orthodox na siyo Haile Selassie.

Alipokuwa katika mahojiano Askofu aliyembatiza Marley, Abuna Yesehaq wa kanisa la Ethiopia Orthodox, alisema Marley alikuwa mtoto wa Mungu tofauti na watu walivyomuona.

Aliendelea kusema “Ugonjwa wake wa kansa ulikuwa sababu kubwa ya yeye yeye kumpokea Bwana Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Watu wengi walidhani alibatizwa kwa sababu alijua angekufa, lakini haikuwa hivyo, alibatizwa kwasababu hakuwa na msukumo kutoka kwa yeyote na alipobatizwa aliikumbatia familia yake na kulia kwa nusu saa.”

Marley alibatizwa tarehe 4 Novemba 1980 na alifariki  21 May 1981 akiwa na miaka 36.

Tukiachana na habari ya Robert Nesta Marley au Bob Marley, Kuna dini ya marastafari na washirika wake tunao mitaani ambapo kwa asilimia kubwa ni vijana, Je dini hii ya marasta wanaamini nini? na rasta zinahusiana vipi na kuvuta Bangi?

MWANZA KUMEKUCHA KWA SHANGWE ZA KUMTUKUZA MUNGU


Monday, February 27, 2012

SAUT Wamwadhimisha Bwana katika Campus Night


Lile Tamasha la kusifu na kuabudu lililokuwa likisubiliwa kwa hamu na wanachuo na wakazi wa Mwanza lijulikanalo kama campus Night, ijumaa iliyopita lilifanyika  katika viwanja vya shule ya msingi Nyamalango iliyoko Nyegezi jijini Mwanza  karibu kabisa na Chuo kikuu cha Mtakatifu Augustine(SAUT).Vikundi kama TAFES SAUT,KingDom Worshipers,CASFETA,HHC Praise and Worship Team pamoja na kihaire Band vilimuadhimisha Bwana Viwanjani hapo.

Maandalizi ya  Tamasha hilo yalifanyika  kwa ushirikiano mkubwa kati ya TAFES-SAUT na kanisa la HIGHWAY OF HOLLINES  linaloongozwa na Akofu Eugine Mulisa. Tofauti na Matamasha mengine Tamasha hili lilikuwea la kihistoria kwa kuwa lilikuwa ni tamasha la kwanza kurushwa LIVE kupitia kituo cha redio cha  ALIVE FM ambapo Nyamiti Kanyola mmoja wa watangazaji wa redio hiyo aliongoza jopo la ufundi kutoka ALIVE FM katika kuhakikisha walioko majumbani wanakutana na ngumu za Mungu.

Mtumishi wa Mungu Askofu Eugine Mulisa akifundisha Neno la Mungu kisha akaongoza idadi kubwa ya watu sala ya toba  baada ya kuamua kumpokea YESU kama Bwana na mwokozi wa Maisha yao.Tofauti na Campus Night zilizowahi kufanyika na Maombezi kuwa ni sehemu tu ya Mahubiri, kilichojiri kwenye Concert hili ni Tofauti kwani waliolipuka Mapepo walikuwa ni wengi mno hivyo kupelekea wahudumu na watumishi kuwa na kazi ya ziada katika kufanya huduma ya Maombezi.

Evelyn Andrew New member wa bend ya KingDom Worshiper na mtangazaji wa Kwa Neema Fm akiwa on stage.


Tafes Saut Praise and Worship Team ikihudumu




Mtumishi wa Mungu Askofu Eugine Mulisa akifanya maombezi


Maombezi yakiendelea




Watumishi wakiendelea na maombezi




Kingdom Woshipers on Stage

You might also like:

MCHUNGAJI THOMAS JAKES AKIWA NA BENJAMIN DUBE NA MKE WAKE.


Pichani anaonekana Kiongozi wa Kanisa la Potters House la nchini Marekani Askofu Thomas Jakes(TD Jakes) akiwa familia ya Baba na Mama Mchungaji Benjamini Dube wa nchini Afrika ya Kusini.


24 February 2012

CHEKA KIBIBLIA NA FREDDY CHAVALA

Mtumishi Freddy Chavala Kuanza Season One Ya Matamasha ya Cheka Tena(Laugh Again Concert ) Tar 4 March 2012,Pale Landmark Hotel,Ubungo,Dsm.



Crown Chavala

Baada ya mafanikio makubwa ya uzinduzi wa matamasha ya Cheka Tena mwishoni mwa mwaka jana, Nov 20 2011 pale Crystall hall ya Blue pearl hotel, Ubungo plaza. Sasa mbeba maono wa Matamasha hayo Mtumishi Freddy Chavala ameamua kuanza rasmi MSIMU WA KWANZA(SEASON ONE) wa matamasha hayo ya stand up comedy Tanzania, na Tamasha la kwanza la LAUGH AGAIN CONCERT mwaka huu litakalofanyika pale Ibungira hall katika ukumbi wa  LANDMARK HOTEL Ubungo river side, jumapili ya kwanza ya march(4th March 2012), kuanzia saa nane na nusu mpaka mbili usiku(2:30pm-8pm). 

Mbali na CROWN CHAVALA,Tamasha hili la Ubungo litawapandisha comedians chipukizi watano ambao ni Senior ABBY, Gerald Mrema, Richard Chidundo, Josephine Lukweto na MC MANU a.k.a Pilipili ya Sherehe toka Dodoma,Makundi mengine ya watu watakaonogesha tamasha hili ni pamoja na kundi maarufu la vijana waimbaji waitwao GLORIOUS CELEBRATION BAND, pia DAR ES SALAAM GOSPEL BAND, VOCAPELLA GROUP, VICTOR ARON,MADAM RUTH &CHRISS na wengine wengi bila kusahau kundi la DANCE.

Glorious Celebration watakuwepo Landmark Hotel wakimsindikiza Chavala
LAUGH AGAIN CONCERT One One litahusisha Stand Up Comedy(Zaidi), pamoja na Acapella, Dance,Sebene,Story telling, Zawadi & Suprises, Open Mic,Drama,na mengine mengi yatokanayo! Mbali na hayo kutakuwa na uzinduzi wa FORUM iitwayo QUALITY-LOVE.com, ambayo itakuwa maalumu kwa ajili ya kujadili maswala ya Upendo safi kwa kina,ubora,upana na ubora wake katika nyanja mbalimbali za maisha ya binadamu. Na kama mambo yataenda kama yalivyopangwa kutazinduliwa kitabu kiitwacho “NO MORE SCHOOL FOR YOU”(Your birth was your Graduation) By FREDY E. CHAVALA.

Kiingilio kwa tamasha hili itakuwa 5000/= kwa tiketi, ambazo zinapatikana Victory Christian Centre(VCC);Tarakea Restaurant(Mwenge),Silver Spoon and Tausi Fashion pale Mlimani City,Global Publisher na Praise Power Radio
Lakini pia mtu anaweza kununua tiketi kwa M-Pesa (0753 883 797) au Tigo Pesa (0713 883797) kwa kutuma 6000/= na atapata tiketi yake mlangoni, lakini hakikisha unatuma pesa kwa namba yako mwenyewe iliyosajiliwa kwa jina lako!

LAUGH AGAIN CONCERT Season One itakuwa na matamasha nane katika mikoa mitano ya hapa nchini kwa kuanzia, Matamasha haya yatafanyika kuanzia March-August/September 2012 katika mikoa ya Dar es salaam(3),Arusha(1),Mwanza(1),Dodoma(2) na Mbeya(1).
Tar 1st April ni ARUSHA 
29th April ni ndani ya COLD CREST HOTEL,Mwanza 
then DSM tena !



 By Crown Chavala,The King of Standup Comedy! Alimaarufu kama President

NENO LAZIMA LIHUBIRIWE

Mchungaji Boazi Sollo Kuunguruma Mbeya


Boaz Sollo

Mtumishi wa Mungu Boaz Sollo kwa sasa amekuwa akisikika sana katika masikio ya watanzania hususani walio karibu na Media, mchungaji Sollo ni kiongozi wa kanisa la lijulikanalo  kama EndTime Harvest Church lenye makazi yake mkoani Iringa. Amekuwa akihubiri injili katika sehemu mbali mbali na hivi karibuni alifanya mkutano wa injili mkoani Dodoma.

Mchungaji Sollo alimpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa Maisha yake mnamo mwaka 1997 na baada ya kuukulia wokovu amekuwa akifundisha na kuhubiri sehemu mbali mbali nje na ndani ya Tanzania.  Kwa upande wa elimu Mch Sollo ni Mhitimu wa shahada ya Theolojia katika chuo kikuu cha Breakthrough Bible College kilichoko nchini Marekani.

Mungu amekuwa akimtumia Mch Sollo kwa ishara kubwa na maajabu ambapo katika mikutano yake na Ibada kanisani kwake watu wengi wamefunguliwa kwa uweza wa Mungu.Tofauti na kuhubiri Mchungaji Sollo ni ni mwandishi na Muimbaji wa nyimbo za injili ambapo mpaka sasa amesharekodi jumla ya Album za muziki wa injili zipatazo tatu.

Kwa sasa  Mtumishi Sollo anajipanga kufanya mkutano mkubwa wa injili jijini Mbeya Kuanzia tarehe 9-03-2012 mpaka tarehe 11-03-2012 katika Viwanja vya Uhasibu. Tunaamini kuwa Yule Mungu aliyeianzisha kazi ndani yake atatokea na kuikamilisha kwa utukufu wake.

You might also like:

23 February 2012

MUNGU ANAINULIWA HATA KWA MICHEZO

Wakristo nchini China wafurahia Mafanikio ya Jeremy Lin



Jeremy Lin kushoto akishoot

Jeremy Lin's ni Raia wa China ambaye kwa sasa yuko nchini Marekani akicheza mpira wa kikapu katika ligi ngumu na maarufu ya mchezo huo iitwayo NBA. Jeremy ameokoka na ame-make headlines kwenye vyombo vingi vya habari nchini Marekani hasa kwa uwezo wake wapo uwanjani, kwa sasa Jeremy anaichezea timu ya New York Knicks.

Wachina wengi wanafurahia mafanikio ya Jeremy kwa kuwa anaitangaza nchi yao,lakini kwa upande wa pili Wakristo walioko nchini China wao wanafurahi mara mbili kwanza wanaona kufanya vizuri kwa Jeremy ni kumtangaza Kristo nchini humo kwa kuwa ukristo umekuwa ukipigwa vita kwa hali ya juu, na pili anaizangaza nchi hiyo.


Jeremy Lin's kipindi akiichezea timu yake ya Chuo

Jeremy kabla hajaingia NBA alikuwa akisoma katika chuo kikuu cha Havard na kuchezea timu ya kikapu ya chuo hicho iitwayo Harvard's basketball team kisha akajiunga na Houston Rockets.Akiwa chuoni hapo alikuwa akiongoza Bible study katika group la watu 80.Hadi kufikia wiki hii Kwa takribani michezo sita mfululizo Jeremy ameweza kuifungia timu yake wastani wa poits 20 kwa kila mchezo kitendo ambacho kinadhihirisha ufanisi wa Mtumishi huyu.

Ndani ya jamii ya wachina wao, hawaamini katika dini, na wengi wa wakristo hususani waliookoka wanakazi kubwa ya kuwaelimisha wenzao ambao dhana ya upagani Imetawala katika fahamu za wachina wengi.kitendo cha Jeremy kukiri wazi kuwa YESU ndiye anayemuwezesha kufikia hapo alipo kwa kiasi kikubwa imeshitua fahamu za wachina juu ya ukristo.

Wiki iliyopita hiki kitu kilimkuta Masihi wa Bwana Jeremy
Alipokuwa akitoa ushuhuda wa maisha yake katika kanisa la River of Life Christian Church lililoko Calif Santa Clara, Jeremy alisema "Everything in my life are blessings from God, I look back and I realize these are His fingerprints all over my story," Lin said, adding that "our true prize ... was something in heaven, not on earth.""I realize I had to learn ... to stop chasing the perishable prizes of this earth ... and give my best effort unto God and trust Him with the results." 

Angalia Mtupo wa mbali(long Shoot) kutoka kwa Jeremy katika moja ya Mechi za timu yake ya New York Knicks

You might

NABII JOSHUA NDANI YA UTUMISHI

2012

Sio Sahihi Kuuhusisha moja kwa moja unabii wa TB Joshua na Uhai wa Rais Mugabe



Prophet Temitope Balogun Joshua

Mwanzoni mwa mwezi huu Nabii wa Mungu kutoka nchini Nigeria Temitope Balogun Joshua(TB JOSHUA)alitabiri kuwa kiongozi mmoja wa Afrika aliyedumu kwa muda mrefu madarakani ataaga dunia ndani ya siku 60 zijazo, baada ya utabiri huo kumekuwa na kauli nyingi zikiongelea utabiri huo huku wananchi wengi wa Zimbabwe wakiwa ni kwanza kuuvalia njuga utabiri huo kwa kuamini kuwa aliyekuwa akisemwa ni Rais wao yaani Robert Mugabe.

Maneno na mijadala mingi baina ya wazimbabwe ilipelekea sehemu kubwa ya Afrika na watu wasioujua ukweli wa utabiri huo kuamini wazi kuwa aliyekuwa akisemwa ni Mzee Mugabe, na hii ni kutokana na Umri wake kuwa umeenda ukilinganisha na viongozi wengine yeyote walioko madarakani katika bara la Afrika. Msemaji wa chama Tawala cha nchini Zimbabwe(ZANU PF) Mh Rugare Gumbo yeye alipoulizwa juu ya utabiri huo alisema “I do not believe some of these prophecies of doom,”

Ikumbukwe kuwa wakati Mtumishi TB JOSHUA akitoa utabiri huo hakusema ni nchi gani wala ni Rais gani japokuwa Mungu alimwambia juu ya hayo na yeye aliwaomba washirika wake wamuombee Rais huyo. Rais Mugabe sio kiongozi pekee aliyeko madarakani ambaye umri wake umeenda, wapo wengi lakini kwa nini kila mtu aliyesikia unabii huu wa Tb Joshua anaamini muhusika ni Mugabe? hilo ni swali ambalo kila mtu mwenye ufahamu angepaswa kujiuliza.


Kutokana na afya yake kuwa sio nzuri kuna kipindi Rais Mugabe kupata msaada wa walinzi wake pindi awapo katika shughuli zake

Ki umri kwa sasa Mugabe anamiaka ipatayo 88,baadhi ya Marais wengine wa Afrika wenye umri mkubwa ni pamoja na Rais wa Senegal Mh Abdoulaye Wade mwenye miaka 85 ambaye anaheshimika sana kisiasa kwa kuwa upande wa upinzani kwa miaka ipatayo ishirini kabla hajaingia madarakani. Mwingine ni Rais wa Kenya Mh Mwai Kibaki mwenye umri wa miaka 81.

katika orodha hii ya wakongwe yumo pia Rais wa Cameroon Mh Paul Biya mwenye umri wa miaka 79, Rais Biya yeye amekuwa kwenye uongozi kwa takribani miongo mitatu na bado hajaonyesha nia ya kuachia madaraka wakati Rais mpya wa Sadc Mh Michael Sata wa Zambia yeye anaumri wa miaka 79 na kwa muda sasa  na ameripotiwa kusumbuliwa na maradhi mbalimbali. Nchini Malawi wamalawi nao wanamuhusisha Rais mkongwe wa nchi hiyo Mh Bingu Mutharika(79) katika kundi hilo na unabii wa Tb Joshua.

Wakati Nabii wa Bwana TB Joshua akitoa unabii huo kanisani kwake alisema na hapa ninamnukuu “We should pray for one African head of state, president against sickness that will likely take life. It is sickness for a long time – being kept in the body for a long time (sic).“God showed me the country and the place but I’m not here to say anything like that. I am still praying to God to deliver the president concerned.”

Swali linarudi kwa nini Mugabe?, kila kona Mugabe? Hili linabaki kuwa ni fumbo japokuwa wengi wanauhusisha unabii huo na afya ya Mugabe ambapo mara kwa mara imeripotiwa kuwa sio nzuri, lakini ukweli unabaki pale pale wengi wa wakongwe hao hapo juu afya zao sio nzuri.

Kibiblia unabii utokao kwa Mungu ni lazima utimie(it shall come to pass), Mungu anabaki kuwa Mungu na hulithibitisha lile alisemalo toka Enzi na Enzi.

MGENDI NDANI YA GEMU LA GOSPEL

Salamu za Jenifer Mgendi kwa Wapenzi wa Muziki wa Injili na Filamu za kikristo



Jenifer Mgendi

Salaam nyingi ziwafikie wapendwa, naamini kwa neema ya Mungu mmeuona mwaka. Mimi pia, namshukuru Mungu.

Nachukua fursa hii kuwajulisha nilipo na ninapokwenda kwa mwaka huu na naomba  kama kawa muwafikishie watanzania na wasomaji wenu kwa ujumla mambo haya. Natanguliza shukurani zangu za dhati.

DHAHABU, Hii ni albamu yenye mkusanyiko wa baadhi ya nyimbo zangu za zamani kama vile Nini?, Nimrudishie nini Bwana, Nitafika lini?, Mbona washangaa njiani. Ulinipa sauti na nyinginezo ambazo zilitamba miaka ya 2001 na kurudi nyuma hadi mwaka 1995. Albamu hii tayari ipo madukani katika mfumo wa audio cd yaani ni ya kusikiliza. Maandalizi ya video hii yanafanyika na panapo manajliwa mwezi Agosti itakuwa imekamilika.

TEKE LA MAMA
, Filamu hii ipo madukani na imewashirikisha watu mbalimbali kama Bahati Bukuku, Christina Matai, Senga, Lucy Komba na Godliver a.k.a Bibi Esta. Sio filamu ya kukosa kuangalia na uzuri wake unaweza kuiangalia ukiwa umetulia na familia yako bila kuwa na wasiwasi wa kuanza kuwatuma watoto dukani ili wasione picha chafu.

SHEREHE ZA MIAKA 15 YA HUDUMA
Panapo majaliwa na Mungu, natarajia kufanya tamasha la kusherehekea na kumshukuru Mungu kwa miaka 15 tangu nianze huduma ya uimbaji. Tamasha au sherehe hiyo inatarajiwa kufanyika tarehe 05 Agosti, 2012 katika ukumbi wa Landmark Hotel.Video ya album ya Dhahabu itazinduuliwa siku hiyo pia.
 Maandalizi ya tamasha hili yanaendelea na litapambwa na waimbaji mbalimbali watakaoimba live siku hiyo. Sio siku ya kukosa na wote wenye mapenzi mema wanaombwa kujitokeza kwa wingi. Tutaendelea kuhabarishana kuhusu tukio hili kadiri siku zinavyoendelea.

ALBAM MPYA, Maandalizi ya album mpya yanaendelea moyoni lakini rasmi kabisa yataanza mara baada ya tamasha la mwezi wa Agosti na album hii mpya inatarajiwa kuingia sokoni mwezi Aprili mwaka 2013, tukijaliwa uzima.

Ni hayo tu ndugu zangu nawatakia siku njema

22 February 2012

WAMWABUDUO HALISI WATAMWABUDU KATIKA ROHO NA KWELI

Benjamin Dube kuachia His New DvD called Healing in His Presence




Nguli wa Muziki wa injili nchini Afrika ya Kusini  Pastor Benjamini Dube ndani ya wiki hii anatarajia kuachia album yake mpya ya DVD HEALING IN HIS PRESENCE. Dube anasadikika kuwa mmoja ya wanamuziki wa injili wenye mafanikio makubwa nchini humo, DvD hii itakuwa ni muendelezo wa Dvd zake nyingine zilizopewa jina Hilo hilo la IN HIS PRESENCE japokuwa hulibadilisha kwa kuliongezea neno kadri aonavyo Vema.

Benjamin Dube ambaye ziara yake na Kekeletso Phoofolo(KEKE) ilifanikiwa kumtangaza keke vilivyo na hatimaye kukubalika nchini humo na nje ya nchi hiyo, mwaka jana alipata nafasi ya kuja nchini Tanzania kwa Mwaliko wa wa Pastor Isack Malonga wakati wa event ya R.I.O.T. Hapa chini ni album yake ya mwisho iliyoitwa WORSHIP IN HIS PRESENCE kabla yah hii mpya iitwayo HEALING IN HIS PRESENCE.


MPAKWA MAFUTA WA BWANA

22, 2012

The Enemy Deceives Us- Bill Graham



Bill Graham


Many jokes are made about the devil, but the devil is no joke. If a short time ago I had talked about Satan to university students, they would have made light of him, but no longer. Students today want to know about the devil, about witchcraft, about the occult. Many people do not know they are turning to Satan.

They are being deluded because, according to Jesus Christ, Satan is the father of lies and the greatest liar of all times. He is called a deceiver. In order to accomplish his purpose, the devil blinds people to their need of Christ. Two forces are at work in our world—the forces of Christ and the forces of the devil—and you are asked to choose

21 February 2012

Tuesday, February 21, 2012

Umetenda Mema – Kambua Shooting si Ya Kitoto


 Kambua

Kambua ni muimbaji wa nyimbo za Injili  mwenye jina kubwa nchini Kenya, alianza kuimba na kupenda nyimbo za Injili alipokuwa mdogo na watu wengi waliona kilichokuwa ndani yake, baadaye mwaka 2005 akaenda kusomea Muziki nchini  Canada chuo cha Kikristo, Calgary. Na katika maisha yake chuoni, alijiunga na band ya chuo Legacy Youth Conference (LYC). Anasema alipokuwa Canada, hawezi kusahau alipochaguliwa kuimba na Angelique Kidjo kwenye tamasha moja.


Kambua ambaye mama yake ni mchungaji, mbali na nyimbo zake kupigwa redioni na kuonekana kwenye TV pia na tuzo alizopokea haachi kusema kwamba maisha yake ameyatoka kwa Bwana Yesu na kusoma Neno lake mara nyingi.

Muimbaji huyu amekuwa akifanya huduma aliyonayo kwa kushirikiana na waimbaji wengine na kuuinua muziki wa Injili kwa kuiwakilisha nchi ya Kenya na hata Afrika mashariki.

                                             Wakati wa Shooting Ya 

Ametamani kuwa sauti ya wanawake na watoto katika kujenga maendeleo ya nchi zinazoendelea, mbali na shughuli za jamii na uimbaji Kambua pia ni mtangazaji wa Citizen TV, kipindi cha Rauka.

Kambua Akiwa anafanya Shooting.
                                                                             Pozz la Ukweli.
     Kazi Ya Shooting si Mchezo, chini kushoto ni redio ya kusikilizia mziki huku ukienda sawa
                                                                        Uzuri Unachangia Muonekano.
                                                        Kambua akiwa mbele ya Kinanda
                                                             Kambua akituma Vocal
                                                                Kitu Quality
                                               Shooting si Mchezo, hapa akiwa na Backer wake.
                                                                  Kazi nzuri ya Kambua.


Baadae Mpango Mzima Ukakamilika Ukawa namna hii.

20 February 2012

MWAKASEGE LIVE BIAFRA KINONDONI DAR.

TELE-SEMINAR LIVE WITH MWAKASEGE THIS SATURDAY FEB 18TH 2012


Mwalimu Christopher Mwakasege 

 Dear Friends,
We are glad to invite you once again to the Live Tele-Seminar in Which
Mwalimu Christopher Mwakasege from Arusha-Tanzania will be teaching and
praying live for all people especially those living in a Diaspora[USA,Europe,Asia ,Australia, Africa ,Canada etc] this February 18th 2012.

This Seminar will be live Teleconferenced all over the world. Distance is not a barrier anymore, Regardless of where you are at, you can still
participate.


DETAILS

WHAT TIME?

USA & CANADA:   9am Central time,  10am Eastern Time, 7am Pacific Time.
ASIA & RUSSIA: 5PM Jerusalum,8pm Karachi,11pm Hong-Kong
AFRICA: 6pm EAT(DAR-TZ), 3pm (Western Africa Time), 4pm(Central African).
EUROPE: 3pm London-UK,4pm Rome,5pm Sophia
AUSTRALIA: 2.00am,Sunday Morning at Sydney.


HOW TO LOG IN ?
Call: 218-895-2851 then Pass-Code; 9102011

Due to the high volume of callers, would advise you to log in even few
minutes ahead of time in order to be there on time.
You keep logging in till you get in. Prayers will start 30-minutes before
the Seminar .

For more information about MANA MINISTRIES you can also visit
www.mwakasege.org  or facebook :diana&christopher mwakasege(mana-ministry).

Looking forward to seeing you on Saturday  and please share with others !
MANA MINISTRIES (USA)
Tel: Toll free :1888-481-6077 //6513340163  OR 255-27-2504289.
Email: info@mikutano.com
Web: www.mikutano.com // www.mwakasege.org

MUME WA ANGELA CHIBALONZA AKIWA NA MKE MPYA SIKU YA NDOA

Pichani ni siku ya ndoa kati aliyekuwa mume muimbaji maarufu wa nyimbo za injili marehemu Angela chibalonza Apostle Elisha Muliri(kushoto mwenye kofia) alipokuwa  akifunga ndoa na mkewe mpenzi Magreth(katikati) mwaka jana nchini Kenya. Apostle Murili ambaye ni kiongozi wa huduma ya Shekinah International church yenye makao makuu yake jijini Nairob

17 February 2012

LIVE RECORDING BONDENI


MUNGU ATUKUZWA RECORDING YA NTOKOZO MBAMBO WA JOYOUS CELEBRATION

Joyous Celebration ni Next Level


Ntokozo akimsifu Mungu usiku wa kuamkia leo wakati wa recording



Wapenzi wa muziki wa injili nchini Afrika kusini waliofika katika live recording ya mwanadada Ntokozo Mbambo wa Mbatha iliyofanyika katika ukumbi wa Gold reef city lyric theatre jijini Johannesburg,wamenukuliwa wakisema kwamba recording hiyo ilikuwa level nyingine uwepo wa Mungu ulifunika ukumbi huo kwani kila jambo lilikwenda vyema na watu kupokea kutoka kwa Mungu zaidi wakimpongeza mwanadada huyo sambamba na mumewe Nqubeko kwa kazi nzuri


Ntokozo ambaye toleo lake la kwanza alilitoa mwaka 2007,amekuwa kati ya nyota wa muziki wa injili nchini Afrika ya kusini kutokana na nyimbo alizoimba kwakutunga yeye mwenyewe nazile za kukopi kutoka kwa waimbaji wengine duniani  akiwa pamoja na kundi la Joyous Celebration ambako kwasasa ndiye mnoaji wa sauti wa kundi hilo huku mumewe akiwa mtayarishi wa muziki wa kundi hilo akishirikiana na kiongozi wa kundi hilo Pastor Mthunzi Namba


Mrs Mbatha alikuwa kwenye kiwango chake cha uimbaji

Khaya Mthethwa mmoja kati ya waimbaji wa Joyous akiimba kwahisia 



katika uzinduzi wa jana Ntokozo alisindikizwa na waimbaji wenzie wa kundi la Joyous ambao wengine walikuwa wapigaji na  back up vocalist na wengine wakiwa watazamaji, kabla ya uzinduzi huo ambao dalili za kuwa lingefanikiwa zilionekana mapema baada ya ticket kuwa sold wiki moja kabla ya recording yenyewe,ambapo Ntokozo aliisimamia recording yake kwa neno kutoka matendo 2;2, ambapo alinukuliwa akisema '' I have something to say through music which is inspired by God. I'm a believer in NOT just in releasing for that sake of releasing an album'' alisema.


Kutoka kushoto Hlengiwe,Kuki(mwimbaji wa zamani wa joyous)pamoja na Zodwa mahlangu sauti ya pili matata ndani ya Joyous 



Nqubeko akiwa anamsifu Mungu wakati wa recording

Ntokozo akimuangalia mumewe wakati akiimba kwenye drums kijana Siyabulela wa joyous akiwa busy huku jicho akiwakodolea wapendanao


Ntokozo pamoja na mumewe Nqubeko mwaka jana walishinda tuzo za sabc crown gospel kwa category za best producer na classic of all time,ambapo mumewe naye anatarajia kuachia dvd yake wakati wowote kutoka sasa ambapo audio yake inayojulikana kwa jina la forever i'll worship inafanya vyema sana nchini humo

Kutoka kushoto Hlengiwe,Mahalia,Lihle pamoja na Sibongiseni



Kitu Live Hiki

Kwenye Joyous ya 15-2

Source: Gospel Kitaa Blogspot.

16 February 2012

VITA VYA KIROHO PART 1.

VITA VYA KIROHO Part 1


 Yohana 10:10 ‘Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu…
 Waefeso 6:10-18 ‘Hatimaye mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake, vaeni silaha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za shetani 12 kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama ; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwngu wa  roho’.

 2 Wakorinto 10: 3-5 ‘Maana ingawa tunaenenda kaitka mwili hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili 4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili,bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome); 5 tukiangusha mawazo na kila kkitu kilichoinuka kijiinuacho kinyume cha elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii kristo.



 Siku zote jambo lolote lile linalotokea kwenye maisha ya mtu katika ulimwengu wa kimwili ujue lilianzia kwenye ulimwengu wa kiroho. Mfano ukiona wanandoa wanatengana ujue walishatengana kwanza katika ulimwengu wa roho ndipo sasa inadhihirika kwenye ulimwengu wa kimwili.  Kwa hiyo siku zote vita kati ya Mkristo na Shetani inapigwa katika ulimwengu wa roho kwanza.   

 Mtu akimshinda shetani na mapepo yake kwenye ulimwengu wa roho ujue hata kwenye ulimwengu wa mwili atashinda. Naam ni katika ulimwengu wa roho ndipo Mungu anapotaka watoto wake tuliokoka tujue namna ya kuvipiga vita dhidi ya shetani. Naam tukishindwa kwenye ulimwengu wa roho na kwenye ulimwengu wa kimwili tutashindwa na tukishinda kwenye ulimwengu wa  roho na kwenye ule wa mwili tutashinda.

 Ukweli huu tunaupata kutoka kwenye andiko la 2Wakorinto 10:3-5, maana Biblia inasema silaha zetu si za mwili, ina maana ni za kiroho, sasa huwezi kutumia silaha za kiroho kupigana vita ya kimwili
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...