About Me

MFAHAMU PRINCE MABISA

Kati ya Wajukuu wa Mzee Kulola alioa nao basi Kwa wale wafuatiliaji wa Muziki wa Injili hapa nchini jina la "Emmanuel Mabisa" haliwezi kuwa halijawahi sikika katika masikio yako. Emmanuel Mabisa ni Mtoto wa nane kati ya Familia ya Watoto tisa waliozaliwa katika himaya ya Mzee Mabisa ambapo watoto wa Kiume ni Sita na Wakike watatu.

Emmanuel Mabisa alijifunza muziki akiwa na umri wa miaka na umri mdogo sana zaidi ya miaka 15 iliyopita ambapo Kaka yake ndiye aliyemfundisha mambo ya upigaji wa Muziki hususan gitaa la Bass.

Katika Huduma ambazo Emmanuel Mabisa anafanya kwa sasa katika Kanisa Uimbaji ndiyo ambayo imekuwa mbele zaidi, kwa sasa Emmanuel Mabisa ni Music Director wa kundi jipya kabisa la Muziki wa Injili lenye jina la Glorious Celebration lenye maskani yake mitaa ya Chang'ombe. Kundi hilo ambalo limeshaza kuwa tishio katika tasnia ya Muziki wa injili linaundwa na vijana wenye nia ya kumtumikia Mungu zaidi. Kundi la Glorious Celebration ilemkwisha shiriki katika Matamasha mbalimbali katika jiji la Dar-es-Salaam. Mbali na kundi hilo Emmanuel Mabisa anafanya kama "Single Artist" ambapo ambapo amekwisha kutoa albam mbili na ile iliyomutangaza zaidi ni ile yenye jina "Muweke Mbele Yesu"

Blog ilipoongea na Emmanuel Mabisa kutaka kujua mbali na shughuli za Muziki anafanya nini kwa sasa, Mabisa alieleza. "Kwa sasa ana Kampuni yake yenye jina la RUMA Company Limited ambayo kwa sasa inafanya kazi za Graphics kama utengenezaji wa Logo, Websites, Blogs,na Music Directions. Maono ya Baadae ya RUMA kuwa na LEBO ya shughuli za Muziki hapa nchini kwa kuwezesha Wanamuziki kuingia katika medani za kimataifa lakini Pia kuandaa Tuzo mbalimbali za Tasnia ya Muziki hapa Tanzania.

Kati ya Vitu ambavyo mwanamuziki Emmanuel Mabisa anapendelea basi Muziki uko ndani ya damu, lakin pia anapendelea ku chat, kubadilishana mawazo na watu wa rika tofauti tofauti, kati ya vitu ambavyo Emmanuel ameiambia Blog hii hapendi kabisaaaaaa kwenye maisha yake basi kudanganya na kudanganywa hataki hata kusikia.

Katika maisha ya kila siku kuna milima na mabonde kuna furaha na huzuni kuna kufanikiwa na kushindwa, Blog ilitaka kufahamu ni jambo gani ambalo hataweza kulisahau katika maisha, Ndipo akajibu kaka ifuatavyo

"Kuondokewa na Baba yangu nikiwa na umri mdogo ni kitu ambacho nimedumu nacho sana kwenye akili zangu. lakini kwa sasa ninamshukuru Mungu ile hali inaniisha na niko salama zaidi kwa sasa", Blog ilipotaka kufahamu ni jambo gani ambalo "lili bamba" sana Mabisa alisema "Albam ya Muweke Mbele Yesu, imeniweke Mbele zaidi katika Maisha, imenitoa kwa kiasi fulani kimauzo tofauti na kazi zingine nilizowahi kufanya.
Blog inatoa Big Up sana kwa The Prince Emmanuel Mabisa, Part 2 ya Step Up itakuwa "The Glorious Celebration" stay tune with me.
Kwa ushauri wa Mambo ya Muziki, ama Kupigiwa ama kutengenezewa Muziki wa aina yoyote Kichwa ndo hiki hapa Emmanuel Mabisa "The Prince"
-------------------------------------------------------------------------------------------------------

Mimi ni Emmanuel Mabisa nimeokoka nampenda Yesu ni music Director wa Glorious Celebration...pia nafanya kazi kama Producer na voko trainer.MUNGU AKUBALIKI asante.
 









Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...