27 April 2013


The Voice Watimiza Miaka 19 Ya Kuundwa Kwao

Kundi la The Voice siku ya Jana limetimiza miaka 19 na kurekodi Live DVD katika Kanisa CCT pale chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Katika anniversary hiyo iliyofana siku ya jana The Voice walifana sana na kukonga nyoyo za wahudhuriaji ambao walikuwa wamefurika ndani na nje ya ukumbi.

Bomby Johnson akiwa kwenye performance 
Baadhi Ya wadau ndani ya Ukumbi
Music Director SamYona
Ma Mc wa Event Harris Kapiga na Papaa Ze blogger
The Voice
 Kama Kawa the Voice wako pouwa
                                           The Voice
                                    Kikazi zaidi

24 April 2013

Step Up.....Paul Clement Mwakanyamale a.k.a Pastor Paul


Kama ilivyo ada ya Blog ilimtafuta mwanamuziki wa Gospel anayekuja kwa kasi katika anga la muziki wa Injili Tanzania ambaye wiki hii anazindua albam yake ya kwanza kabisa ya Umeniita.


Ze Blogger kama kawa akanyanyua simu kumsaka Pastor Paul....ngriiiiiiiiiiiiiii, ngriiiiiiiiii

Ze Blogger: Hallo, Hallo Paul Bwana asifiwe.

Pastor Paul:  Amen, Papaa za Wewe

Ze Blogger: Kwema, Kaka moja kwa moja Uko hewani na Blog, unaweza tujuza Majina yako Kamili??

Pastor Paul: Majina yangu Kamili ni Paul Clement Mwakanyamale… mtoto wa watatu kuzaliwa kati ya wanne katika familia ya Mzee Mwakanyamale.

 Ze Blogger:Kwanini kuimba zaidi ya kupiga?
Pastor Paul:Kwanza napenda kuimba Mwanzoni niliona kama kuimba ni njia ya kujifariji kutokana na matizo mengi niliyokuwa nayo katika     kukua kwangu… lakini baadaye nikagundua kuwa kuimba ndo huduma hasa Mungu aliyonipa kufanya ili kuwagusa wengi 
zaidi

 Ze Blogger: Safari ya Maisha ya Muziki kwako ilianzia wapi?

Pastor Paul: Nilifundishwa kuimba na Ben Paul ambaye ni muimbaji wa bongo fleva… nilipenda sana anvyoimba, nilikuwa form two by then… nilikuwa naimba mwenyewe nyumbani kwaajili ya kujifariji.. sikuwa na wazo kwamba kunasiku nitaimba kanisani na kwenye concert kubwa… hiyo ilikuwa ni kwaajili yangu mwenyewe. lakini nikaaanza kuimba kwenye matukio ya shule kama graduation na vikundi vya dini kama casfeta na ukwata. Lakini hakuna mtu aliyekuwa anatambua hasa ni nini nilichonacho, nikaendelea tu.Mzee wangu (baba) alikuwa hapendi… ananizuia kufanya mazoezi… nikibeba kinanda toka kanisani kuja nacho nyumbani anazuia.

Nilipofoka form three mwishoni ndio nikaanza kuimba kanisani.. Calvary kwa mchungaji Marko (babaake John Marco) kule keko…nikawa najichanganya na kwenye makanisa mengine kama winners n.k.Nilipomaliza Form four 2010.. ndipo Emmanuel Mabisa aliponitafuta kuniomba nijiunge na kundi la Glorious Celebration. 2o11 kundi la messengers waliniomba kuongeza nguvu kwenye kundi lao kwenye ziara yao nchini Korea.. Lakini baba yangu alizuia nisiende…

2011 tulifanya álbum ya kwanza na Glorious Celebration "Niguse" ambayo ililitambulisha Glorious na kunitambulisha mimi pia ambapo niliimba wimbo wa Juu Ya Mataifa Yote… Mpaka sasa ni mimi ni muimbaji wa Glorious Worship Team.

 Ze Blogger:Kwanini umeamua kufanya Album yako nje ya GWT?

Pastor Paul: Kwanza ninaaamini kuna kitu Mungu anacho kwa mimi kama Paul(kuna maono ya kundi lakini kuna maono binafsi pia… lakini na pia huu ndio ulikuwa wakati sahihi wa album hii kutoka… maana nimekuwa nikistruggle kutoa hii album kwa miaka minne lakini haikuwezekana… nimeshairekodi hii album kama mara nne lakini kila mara ilikuwa ikiharibika au files zinapotea au kuliwa na virus…. 

 Ze Blogger:Albam ya Umeniita Ina jumla Ya nyimbo ngapi? 

 Pastor Paul: Album hii ni ya kwanza ina nyimbo 8. Kwanini umeniita?!!!! hahahaa!!! Jina lenyewe limejielezea… Wimbo huu nimeutunga sio siku nyingi sana zilizopiata… na niliutunga baada ya kutambua kuwa Mungu mwenyewe ameniita nimtumikie… Katika yote niliyopitia nilijua kuwa nilipita kwa makusudi nijifunze ili nimtumikie..

 Ze Blogger:  Kuna Changamoto ya wanamuziki kujisimamia wewe umejipangaje katika hili.

Pastor Paul: kwanza ni kweli changamoto ipo… na mie nimeitambua na nikaona sitaweza kujisimamia mwenyewe…. nikaamua kutafuta kampuni ya kusimamia kazi yangu. Kazi inasimamiwa na Mancon E.A Ltd. Chini ya Director Prosper Mwakitalima.

 Ze Blogger:Mara nyingi sana nimeona wanamuziki wanavuma miaka michache sana na wanakuwa hawana Malengo ya baadaye wee umejipangaje?

Pastor Paul:kwanza lengo kubwa ni kufikia sio Tanzania peke yake bali ulimwengu mzima… Tanzania ni mwanzo tuu.Pili kuwa na chuo cha muziki, studio ya Audio na video
na pia malengo baadye ni kufanya filamu pia za Gospel… sitaishia kuimba peke yake!
Lakini mwisho kabisa ni kuwa mchungaji…. Nasikia wito saaana!!!

 Ze Blogger: :Swali la kizushi… kuna issue ya wadada maana najua kwa umri wako na anointing uliyokuwa nayo nadhani una changamoto ya kukabiliana nao unasemaje!!!

Pastor Paul:Kwangu mie hizo ni simple sana… Kikubwa ni kujitambua wewe ni nanai na unafanya nini hivyo vitu haviwezi vikakusumbua. Licha ya hivyo Mungu anatubeba saaana nikimaanisha Mungu anatusaidia….. Ni neema!!!
Ze Blogger: Watu watarajie nini jpili??

Pastor Paul:Najua wengine wanatarajia Album waisikilize waone wakosoe… lakini mie nina kitu tofauti na hicho… Naamini Mungu atafanya jambo la tofauti saana siku hiyo!!
Na yeyote ajaye.. aje amwabudu Mungu na kumsifu Mungu… na kama alikuwa na tatizo lolote Mungu atamtokea katika maisha yake…

Ze Blogger: wanamuzikia unawakubali/wanakuinspire bongo.

Pastor Paul: MpeloKapama na Joel wa Glorious Celebration na Nje ya TZ - Marvin Sapp na Ephraim Sekele


Ze Blogger: Watu wengi wanakufananisha na Detrick Hadon je wewe ni mfuatiliaji sana wa kazi zake ama imetokea tu???


Pastor Paul: kweli ananiispire sana… uimbaji wake na ile kwamba ni mchungaji kijana saana aniispire sana.

Ze Blogger: Wimbo wa "umenifanya ibada" ulioimba na Glorious umegusa mioyo ya wengi saaana… ilikuwaje kuwaje ukatunga wimbo Powerful hivyo??

Pastor Paul:Huo wimbo Mungu aliongea nami direct kabisa… Nilikuwa kwenye maombi nikiomba Mungu anifundishe kumwabudu… nikiwa naomba nikasikia sauti ikiniambia "sitakufundisha namna ya kuniabudu… bali nitakufanya wewe kuwa mwabuduji" na "sitakufundisha ibada nitakufanya wewe kuwa ibada"… huo ndo mwanzo wake!!!

Mchaka Mchaka wa Africa Gospel Music Awards 2013 Yaanza Rasmi

Kwa Mara ya nne mfululizo Africa Gospel Music Awards imechukua Mkondo wake.
Ule Mchakato ambao Mwaka Jana Bloggers Wa Tanzania waliubebea Bango wa Africa Music Awards baada ya Mwanamuziki Christina Shusho Kuingia katika Kinyang'anyiro hicho mwaka huu umeanza rasmi.

Taarifa kupitia tovuti ya Africa Gospel Music Awards na Facebook Page Wametoa Press Release kutaarifu Jamii Kuwa Mchakato huo umezinduliwa rasmi kwa ajili ya kusaka Wanamuziki Bora wa Injili Africa kuanzia tarehe 22 April, 2013.

Utaratibu Uko Kama Ifuatavyo.

Tarehe 22 April Mpaka tarehe 13 May, 2013 Kila Mwananchi anaruhusiwa kupendekeza Jina ambalo anaona linafaa kuingia katika kinyang'anyiro hicho. Njia ni rahisi tu unatuma email kwenda nominations@africagospelawards.com  unaandika jina unalodhani linafaa.

Kuanzia tarehe 1 June mpaka 30 June Kutakuwa Kuna Kupiga Kura kwa Majina yatakayokuwa yameingia katika Kinyang'anyiro hicho ili kupata Washindi katika Categories zifuatazo.


1.DISCOVERY OF THE YEAR
2.ARTISTE OF THE YEAR EUROPE
3.ARTISTE OF THE YEAR EAST AFRICA
4.ARTISTE OFTHE YEAR WEST AFRICA
5.ARTISTE OF THE YEAR NORTH AFRICA/MIDDLE EAST
6.ARTISTE OF THE YEAR SOUTHERN AFRICA
7.ARTISTE OF THE YEAR CENTRAL AFRICA
8.ARTISTE OF THE YEAR USA/CANADA
9.ARTISTE OF THE YEAR AUSTRALIA/ASIA PACIFIC
10.SONG OF THE YEAR
11.ALBUM OF THE YEAR      
12.MALE ARTISTE OF THE YEAR
13.FEMALE ARTISTE OF THE YEAR
14.MUSIC PRODUCER OF THE YEAR
15.RADIO PROGRAM OF THE YEAR
16.MUSIC VIDEO OF THE YEAR
17.  EVENT OF THE YEAR
18.  AFRO JAZZ/INSTRUMENTAL MUSICIAN OF THE YEAR
19.GOSPEL RADIO PRESENTER OF THE YEAR
20.GOSPEL TV PROGRAM OF THE YEAR
21.GOSPEL TV PRESENTER OF THE YEAR
22.GROUP /CHOIR OF THE YEAR

Mwaka Juzi na Mwaka Jana Mwanamuziki Christina Shusho aliingia katika Kinyang'anyiro hicho. Ambapo Kampeni hiyo Ilipewa jila na "Viva Shusho, Viva Tanzania"
Mwaka Jana Wakati Wa Campaign za Shusho ndani Ya Clouds Radio

Bloggers nza Shusho Ndani Ya Clouds FM

Campaign Manager Ze Blogger akiwa na Shusho

Kaka Mkubwa Pastor Harris Kapiga akiwa na Kikosi Kazi.
Mwaka huu Nani Kuiwakilisha Tanzania??

19 April 2013

ALIKUFA KWA AJILI YA DHAMBI ZETU
jesus_on_cross.jpg

PIA

NI

MCHUNGAJI WA WAISHA YETU.

497033.jpg

AMEN.

A Brief History of Christianity

 

By Michael Faber

Genealogy is a hot topic these days.  People are excited to find out who their ancestors are and how they came to be where and who they are.  And this is an important pursuit.  Knowing one’s family story gives one a sense of belonging and continuity within a family.  But the family story is not the only story.  Christians have a story, as well.  And understanding Christianity’s story is important in understanding how Christianity came to be what it is today and how present day Christians participate in that story.  This article presents a very brief overview of that story: The story of Christianity, incarnation to eternity.
The story begins as God comes to men as a man.  He took to Himself a human nature and walked among us.  His name was Jesus.  He was born in Bethlehem to a virgin, and grew up in a small town in Israel named Nazareth.  When He grew up, He performed many miraculous signs, and preached with the authority of God.  Many came and followed Him.  But not everyone.  Jesus’ enemies, the leaders of Israel, were so threatened by Him that they plotted to arrest Him, charge Him falsely, and put Him to death for blasphemy.
But this was all part of God’s plan.  Jesus was put to death by crucifixion.  But death could not hold Him.  Three days later, Jesus was resurrected, and appeared to His disciples.  He ate some fish to demonstrate that it was, in fact, Him, resurrected in His body, wounds and all.  After several days, Jesus commanded them to wait for the Holy Spirit to come in power, and then He returned to heaven.
On the day we now call Pentecost, the Holy Spirit came, and Jesus disciples spoke in languages they could not understand, and preached the good news of salvation to the crowds in Israel.  Three thousand came to believe in Christ that day. And thus the church was born.
Of course, this isn’t the end of the story, but the beginning.  The Church does not exactly live happily ever after.  Not yet, anyway.  The church is born into a time when those around them did not want them.  The Church was persecuted from the beginning; first by the Jewish leaders of Israel who rejected Christ as messiah; then by Jewish synagogues around the world; and finally by the Roman government, who determined Christianity to be an illegal religion, and often imprisoned or killed those who claimed to be Christians.
Then the world literally changed overnight.  Constantine, the Emperor of Rome became a Christian in 323 AD, and declared Christianity to be the religion of the Empire.  Suddenly it was no longer a crime to be a Christian, but a crime NOT to be one.  Everything was turned on its head.  Up until this time, one of the major Christian issues was what to do with those who believed, but either gave up being Christians because of persecution or publicly declared that they were not Christians in order to avoid persecution.  Up until this time, baptisms were made immediately upon profession of faith because there was no question that the individual believed because of the threat of persecution.  Church was held in households and was lead by house leaders.  Communion was served as a meal.
Now people were claiming to be Christians simply because Rome demanded it.  People wanted to be baptized to obey the law.  The problem wasn’t those who rejected their faith, but those who claimed it out of duty to Rome or to fit in, and had no interest in being faithful to Christ.  Communion wasn’t a mail shared by a household, but a massive event endured by the entire empire.  In a sense, Christianity had gone from persecuted to persecutor, albeit the Roman government was persecuting, but it was not long before the Roman government and the Church became indistinguishable.
In spite of these massive changes, this period of time is one we might call the Time of the Creeds.  Over the next 450 years or so, the Church would enact seven major creeds, which define fundamentally what the Church believes: Nicea (325), Constantinople (381), Ephesus (431), Chalcedon (451), Constantinople II (553), Constantinople III (680), Nicea II (787).  These creeds deal with the nature of God, the natures of Christ, and the acceptability of icons in worship.  If you want to understand some of the underlying theology of the Church, these creeds are a great place to start.
The Church, in spite of its theological struggles, remained one Church for a thousand years.  But in 1054, the Western Church, which we now know as the Roman Catholic Church (RCC) made a minor modification to one of the creeds, and the Eastern Church, which were comprised of the other major Churches, which we now call the Eastern Orthodox Church, did not agree with it.  So bitter was the dispute over the Filoique that each side excommunicated the bishops of the other church, and the church was split in two: East and West.
The two churches remained two churches until the 1500s until an Augustinian Monk by the name of Martin Luther began to have some significant differences with the RCC.  He began to write and engage other church leaders on these matters, and created quite a stir.  Luther wanted to have a debate with the RCC about these matters, and created 95 theses, or statements to be debated.  When the RCC refused, Martin Luther grabbed a hammer and nailed these 95 theses to the door of the local church.  Needless to say that the RCC was not happy about Luther’s actions, and eventually excommunicated him.
Luther had developed quite a following in Germany, and the people there rallied to him, and they formed their own church, to protest the problems within the RCC.  This began what we now call the Protestant movement, of which the first church was the Lutheran Church, named after Martin Luther.  Other leaders and churches would follow suit.  In Switzerland, John Calvin began the theological tradition that is known as Calvinism, and is followed by many Protestant churches.  In the Netherlands, Arminius began his theological tradition.  The Protestant Church has grown to become a third wing of the church, comprising many denominations and independent churches that have their roots directly or indirectly in the RCC, but remain apart in protest of theological and practical problems.
That brings us to today.  The church remains divided, coping with myriad disputes between its groups.  Yet, there remains a fundamental element of unity in the church surrounding Christ and the essential beliefs that make us all Christians.  It is now our turn to write a chapter in Christianity’s story.  Perhaps is it time to put aside our differences and make it our shared priority to represent the body of Christ as one body united in the purpose of reaching the world with the gospel, so that salvation might come to all men, and we might all spend eternity in the glory and majesty that is Christ our savior.

17 April 2013

MAZISHI YA WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA UINGEREZA MARGRET THATCHER YAFANYIKA MJINI LONDON

Jeneza la Margaret Thatcher 
VIONGOZI na watu maarufu katika nchi 170 kote duniani wako mjini London kuhudhuria mazishi ya waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Margret Thatcher maarufu kama Iron Lady. 
Maelfu ya watu mjini London wamepiga kambi tangu usiku wa wa kuamkia leo katika kanisa katoliki la St. Paul, kuliona jeneza la Margret Thatcher lililofinikwa kwa bendera ya Uingereza, shada kubwa la maua juu yake na kusindikizwa na jeshi la nchi hiyo.
Waombolezaji katika mazishi ya Margaret Thatcher 
  Waombolezaji katika mazishi ya Margaret Thatcher.
 
Anthony Boutall mkaazi wa London aliye na umri wa miaka 25 amesema ameamka na kufika nje ya kanisa hilo kushuhudia mazishi ya shujaa ambaye aliibeba na kuinua Uingereza. 

Bendera kote nchini humo zimepeperushwa nusu mlingoti kutoa heshima kwa mwendazake Margret Thatcher aliyekuwa akiugua kiharusi na kufariki tarehe 8 mwezi huu akiwa na umri wa miaka 87.

Sio wote wanaoomboleza kifo cha Thatcher
Hata hivyo sio wote nchini Uingereza wanaoomboleza kifo cha bibi wa Chuma-Iron Lady, Mamia ya wapinzani wa kisiasa wamesema watanyamaa kimya kwa dakika moja na kulipa mgongo jeneza hilo litakapopitishwa.
Waandamanaji katika mazishi ya Thatcher 
  Waandamanaji katika mazishi ya Thatcher.
 
Kwa upande wake Henry Page amabye ni mwalimu msataafu aliyebeba bango lililopinga mamilioni ya fedha yaliotumika kuandaa mazishi ya Thatcher, amesema gharama ya juu haipaswi kutumika katika mazishi ya mtu ambaye katika uongozi wake aliwagawanya waingereza katika misingi ya kijamii na hata kiuchumi.
Takriban dola milioni 15 zimetumika katika mazishi hayo.

Jeneza la Margret Thatcher kwa sasa linapitishwa kutoka katika majengo ya bunge, kupelekwa katika kanisa la St. Clement Danes, kisha kuwekwa katika msafara wa farasi na kuanza kusafirishwa tena pole pole hadi katika kanisa katoliki la St Paul ambako wageni waalikwa takriban 2300 akiwemo Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza watakuwepo kupokea mwili huo.

Usalama waimarishwa.
Polisi takriban 4000 wamesambazwa kote mjini humo kuimarisha usalama. Kiongozi huyo wa zamani ambaye alipewa jina hilo la Bibi wa Chuma- Iron Lady aliibadilisha Uingereza katika kipindi cha miaka 11 alichoongoza kama waziri mkuu wa nchi hiyo kuanzia mwaka wa 1979 hadi 1990.
Usalama waimarishwa  
  Usalama waimarishwa.
 
Wanaohudhuria mazishi ya Thatcher ni pamoja na Malkia Elizabeth wa Uingereza, mumewe Prince Philip, Mawaziri wakuu 11 kutoka mataifa mbali mbali duniani, waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani Henry Kissinger na makamu wa zamani wa rais wa Marekani Dick Cheney.

Wageni maarufu waliotoa udhuru wa kutohudhuria mazishi hayo ni kiongozi wa zamani wa kisovieti Mikhail Gorbachev na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel atawakilishwa waziri wake wa mambo ya nje.

Hata hivyo familia ya Bill Clinton na George Bush zilikataa kuhudhuria mazishi hayo.
KEKE PHOOFOLO

http://www.youtube.com/watch?v=S8rt_qyE3JA

Join Mr Keke in glorifying God.
 
Pia jiandae na album yake mpya aliyoifanya mwaka jana desemba.
!!BarikiwA!!
  

16 April 2013


Heaven flavour ni mashindano ya kusaka vipaji vya waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania , Fuatilia kipindi hiki Tv Sibuka kila jumapili saa mbili usiku hadi saa tatu usiku na marudio ni kila jumanne saa tisa alasili hadi saa kumi jioni. Pia unaweza kutembelea Page na kui Like.http://www.facebook.com/pages/Heaven-Flavour-Talents/565575056816222?ref=hl  Nautapata mengi kuhusu hiki kipindi.
Mpiga Bass Wa Glorious Worship Team avamiwa na Vibaka na Kujeruhiwa.

Mwanamuziki anayepiga bass guitar katika kundi la GWT mwenye Jina la Emmanuel almaarifu ImmaBass amevamiwa na vibaka usiku wa jana alipokuwa njiani kuelekea nyumbani akitoka kwenye mazoezi.

Taarifa ambazo blog imezipata ImmaBass alikimbizwa katika hospital ya Kairuki na Kushonwa nyuzi 8 usoni. ImmaBass alipata majeraha hayo alipokuwa akipambana na vibaka hao waliokuwa wamemvamia.

ImmaBass kwa Sasa anaendelea vizuri, unaweza kushiriki kwa kumuombea pia, na sms ya faraja ama Tigo Pesa 0717561351.

08 April 2013


Tamasha La Pasaka La Konga Nyoyo ndani ya Jiji la Dar-es-Salaam

Pamoja na Mvua Kubwa iliyonyesha leo katika jiji la Dar-es-Salaam Maelfu Ya Wakazi wa Jiji la Dar wamejitokeza katika Tamasha la Pasaka lililofanyika katika Uwanja wa Taifa.

Tamasha Pasaka ni Tamasha linalofanyika Kila Mwaka mara moja katika Msimu wa Pasaka ambapo wanamuziki wa nje na ndani ya Tanzania wanakuwa na muda wa pamoja wa Kusifu na Kumwabudu Mungu.


Mwaka 2013 Kauli Mbiu ya Tamasha ni Amani na Utulivu ambapo fedha zitakazopatikana ni maalum kwa ajili ya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Katika siku ya leo Mgeni rasmi alikuwa ni Mhe. Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye mara kadhaa alipata shuruba ya kupigiwa makelele mara kwa mara kutokana na kukatika katika kwa umeme mara kwa mara.


Mwanamuzi Mwalikwa wa Mwaka huu Kutoka Africa ya Kusini ni Sipho Makabane ambaye jioni ya leo amefanya Performance ya nyimbo 10 Mfululizo ndani ya uwanja huo na Kukonga nyoyo za watu waliohudhuria Tamasha la leo. Malkia wa Muziki wa Injili Tanzania Rose Muhando alifanya kile ambacho kilitarajiwa na Wakazi wa Jiji kwa Kuimba wimbo wa Utamu wa Yesu ulioombwa na Mhe. Mgeni rasmi.


Wanamuziki Wengine waliokuwepo siku ya leo ni Christ Ambassadors kutoka Rwanda, Solomon Mukubwa, Anastazia Mukabwa, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, John Lisu, Faraja Mtabobwa na Glorious Worship Team.

Waimbaji Wa Christ Ambassadors kutoka Rwanda walishuka Kutoka Jukwaani na kugusa wanakazi wa jiji la dar na wimbo wao "Kwetu Pazuri" 

Mwanamuziki Wa Injili wa Tanzania Upendo Kilahiro akienda sawa Siku Ya Leo

Upendo Nkone akiwa Jukwaaani
Anastazia Mukabwa kutoka Kenya akiwa na Rose Muhando ambao kwa pamoja wameimba wimbo wa "Kiatu Kivue"
 Christ Ambassadors Choir wakiwa tayari kwa ajili ya Kazi. 
Solomoni Mukubwa akiwa anapadna Stejini tayari kwa ajili ya Kuimba siku ya leo

Ephrahim Sekeleti Mwuimbaji Kutoka Zambia akiwa George Mpella na Hudson Kamoga
Glorious Worship Team wakienda Sawa siku Ya Leo
Malkia wa Muziki wa Injili Rose Muhando akiwa Kikazi Zaidi

Ephrahim Sekeleti akienda Sawa Siku Ya leo
Sipho Makabane akiwa kikazi Zaidi siku Ya leo
Sehemu Ya Umati Wa Watu

Rose akiendelea na Kazi huku Waandishi na Walinzi wakiwa wamemzunguka
Sipho akijiandaa kuingia Jukwaani
Pole Pole akisogelea Umati Wa watu
Koti Likawa Zito
Kikazi Zaidi
Hapa wakitengeneza Tangazo la Chomoza
Bon Mwaitege akiwa mbele ya Camera Man Ray wa Clouds Tv.
Sipho akienda Sawa na Wananchi siku ya leo
Watu Nyomiiiii
Wakati Sipho akiimba ni kama ilikuwa Mchaka Mchaka Kulia ni Anastazia, Rose Muhando Upendo Nkone na Solomon wakimpa Support Sipho.
John  Lisu 

Without Caption 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...