24 April 2013

Step Up.....Paul Clement Mwakanyamale a.k.a Pastor Paul


Kama ilivyo ada ya Blog ilimtafuta mwanamuziki wa Gospel anayekuja kwa kasi katika anga la muziki wa Injili Tanzania ambaye wiki hii anazindua albam yake ya kwanza kabisa ya Umeniita.


Ze Blogger kama kawa akanyanyua simu kumsaka Pastor Paul....ngriiiiiiiiiiiiiii, ngriiiiiiiiii

Ze Blogger: Hallo, Hallo Paul Bwana asifiwe.

Pastor Paul:  Amen, Papaa za Wewe

Ze Blogger: Kwema, Kaka moja kwa moja Uko hewani na Blog, unaweza tujuza Majina yako Kamili??

Pastor Paul: Majina yangu Kamili ni Paul Clement Mwakanyamale… mtoto wa watatu kuzaliwa kati ya wanne katika familia ya Mzee Mwakanyamale.

 Ze Blogger:Kwanini kuimba zaidi ya kupiga?
Pastor Paul:Kwanza napenda kuimba Mwanzoni niliona kama kuimba ni njia ya kujifariji kutokana na matizo mengi niliyokuwa nayo katika     kukua kwangu… lakini baadaye nikagundua kuwa kuimba ndo huduma hasa Mungu aliyonipa kufanya ili kuwagusa wengi 
zaidi

 Ze Blogger: Safari ya Maisha ya Muziki kwako ilianzia wapi?

Pastor Paul: Nilifundishwa kuimba na Ben Paul ambaye ni muimbaji wa bongo fleva… nilipenda sana anvyoimba, nilikuwa form two by then… nilikuwa naimba mwenyewe nyumbani kwaajili ya kujifariji.. sikuwa na wazo kwamba kunasiku nitaimba kanisani na kwenye concert kubwa… hiyo ilikuwa ni kwaajili yangu mwenyewe. lakini nikaaanza kuimba kwenye matukio ya shule kama graduation na vikundi vya dini kama casfeta na ukwata. Lakini hakuna mtu aliyekuwa anatambua hasa ni nini nilichonacho, nikaendelea tu.Mzee wangu (baba) alikuwa hapendi… ananizuia kufanya mazoezi… nikibeba kinanda toka kanisani kuja nacho nyumbani anazuia.

Nilipofoka form three mwishoni ndio nikaanza kuimba kanisani.. Calvary kwa mchungaji Marko (babaake John Marco) kule keko…nikawa najichanganya na kwenye makanisa mengine kama winners n.k.Nilipomaliza Form four 2010.. ndipo Emmanuel Mabisa aliponitafuta kuniomba nijiunge na kundi la Glorious Celebration. 2o11 kundi la messengers waliniomba kuongeza nguvu kwenye kundi lao kwenye ziara yao nchini Korea.. Lakini baba yangu alizuia nisiende…

2011 tulifanya álbum ya kwanza na Glorious Celebration "Niguse" ambayo ililitambulisha Glorious na kunitambulisha mimi pia ambapo niliimba wimbo wa Juu Ya Mataifa Yote… Mpaka sasa ni mimi ni muimbaji wa Glorious Worship Team.

 Ze Blogger:Kwanini umeamua kufanya Album yako nje ya GWT?

Pastor Paul: Kwanza ninaaamini kuna kitu Mungu anacho kwa mimi kama Paul(kuna maono ya kundi lakini kuna maono binafsi pia… lakini na pia huu ndio ulikuwa wakati sahihi wa album hii kutoka… maana nimekuwa nikistruggle kutoa hii album kwa miaka minne lakini haikuwezekana… nimeshairekodi hii album kama mara nne lakini kila mara ilikuwa ikiharibika au files zinapotea au kuliwa na virus…. 

 Ze Blogger:Albam ya Umeniita Ina jumla Ya nyimbo ngapi? 

 Pastor Paul: Album hii ni ya kwanza ina nyimbo 8. Kwanini umeniita?!!!! hahahaa!!! Jina lenyewe limejielezea… Wimbo huu nimeutunga sio siku nyingi sana zilizopiata… na niliutunga baada ya kutambua kuwa Mungu mwenyewe ameniita nimtumikie… Katika yote niliyopitia nilijua kuwa nilipita kwa makusudi nijifunze ili nimtumikie..

 Ze Blogger:  Kuna Changamoto ya wanamuziki kujisimamia wewe umejipangaje katika hili.

Pastor Paul: kwanza ni kweli changamoto ipo… na mie nimeitambua na nikaona sitaweza kujisimamia mwenyewe…. nikaamua kutafuta kampuni ya kusimamia kazi yangu. Kazi inasimamiwa na Mancon E.A Ltd. Chini ya Director Prosper Mwakitalima.

 Ze Blogger:Mara nyingi sana nimeona wanamuziki wanavuma miaka michache sana na wanakuwa hawana Malengo ya baadaye wee umejipangaje?

Pastor Paul:kwanza lengo kubwa ni kufikia sio Tanzania peke yake bali ulimwengu mzima… Tanzania ni mwanzo tuu.Pili kuwa na chuo cha muziki, studio ya Audio na video
na pia malengo baadye ni kufanya filamu pia za Gospel… sitaishia kuimba peke yake!
Lakini mwisho kabisa ni kuwa mchungaji…. Nasikia wito saaana!!!

 Ze Blogger: :Swali la kizushi… kuna issue ya wadada maana najua kwa umri wako na anointing uliyokuwa nayo nadhani una changamoto ya kukabiliana nao unasemaje!!!

Pastor Paul:Kwangu mie hizo ni simple sana… Kikubwa ni kujitambua wewe ni nanai na unafanya nini hivyo vitu haviwezi vikakusumbua. Licha ya hivyo Mungu anatubeba saaana nikimaanisha Mungu anatusaidia….. Ni neema!!!
Ze Blogger: Watu watarajie nini jpili??

Pastor Paul:Najua wengine wanatarajia Album waisikilize waone wakosoe… lakini mie nina kitu tofauti na hicho… Naamini Mungu atafanya jambo la tofauti saana siku hiyo!!
Na yeyote ajaye.. aje amwabudu Mungu na kumsifu Mungu… na kama alikuwa na tatizo lolote Mungu atamtokea katika maisha yake…

Ze Blogger: wanamuzikia unawakubali/wanakuinspire bongo.

Pastor Paul: MpeloKapama na Joel wa Glorious Celebration na Nje ya TZ - Marvin Sapp na Ephraim Sekele


Ze Blogger: Watu wengi wanakufananisha na Detrick Hadon je wewe ni mfuatiliaji sana wa kazi zake ama imetokea tu???


Pastor Paul: kweli ananiispire sana… uimbaji wake na ile kwamba ni mchungaji kijana saana aniispire sana.

Ze Blogger: Wimbo wa "umenifanya ibada" ulioimba na Glorious umegusa mioyo ya wengi saaana… ilikuwaje kuwaje ukatunga wimbo Powerful hivyo??

Pastor Paul:Huo wimbo Mungu aliongea nami direct kabisa… Nilikuwa kwenye maombi nikiomba Mungu anifundishe kumwabudu… nikiwa naomba nikasikia sauti ikiniambia "sitakufundisha namna ya kuniabudu… bali nitakufanya wewe kuwa mwabuduji" na "sitakufundisha ibada nitakufanya wewe kuwa ibada"… huo ndo mwanzo wake!!!

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...