17 June 2012

Sunday, June 17, 2012

Baada Ya Facebook na Tweeter, Viva Shusho Viva Tanzania Campaign Yahamia Redioni

Baada ya effort kubwa wiki inayoisha kuelekezwa katika Social Media, weekend hii nguvu iliekezwa katika Radio mbali mbali hapa nchini kwa ajili ya Campaign ya kufanikisha Mwanamuziki Pekee Wa Injili Tanzania aliyeingia katika Tuzo za Mwanamuziki Bora wa Injili kuweza Kutwaa tuzo hizo.

Mwanamuziki huyo Christina Shusho ambaye mpaka sasa amefanya Interview na Radio Ushindi FM yenye makazi yake Mkoani Mbeya, ameshafanya Interview na WAPO Radio, na leo Campaign zimeendelea ndani ya Clouds FM na Praise Power FM.

Nia na Madhumuni ya Campaign ni kuhakikisha Mwanamuziki Christina Shusho kutwaa tuzo ya "Mwanamuziki Bora wa Kike Barani Africa" na "Mwanamuziki Bora Kutoka Africa Mashariki"

Ili Kumpigia Shusho Kura, bonyeza www.africagospelmusicawards.com , then bonyeza "Nominees 2012" Kisha Fuata Maelekezo.
 blogger Victor wa www.hossanainc.blogspot.com akiwa amepoz leo kwenye Ofisi za Clouds kabla ya Kuingia kwenye Interview ya Shusho.
 Papaa Ze Blogger akiwa anasoma soma nondoz kabla ya kuingia kwenye interview ya Clouds FM
 Shusho Kushoto, Victor Kulia wakiwa ndani ya Clouds FM asubuhi ya leo
 Kulia ni shusho, Kati ni Victor na kushoto ni Papaa Ze Blogger ndani ya Clouds FM.
 Pastor Harris Kapiga akiwa Kikazi zaidi asubuhi ya leo ndani ya GT ya Clouds FM.
 Nimetoka Mbali sana na hawa Kigoma People aiseee
 Bloggers ndani ya Clouds FM asubuhi ya leo tukiwa kikazi zaidi
 Hapa Timu iliamia Praise Power FM Mchana wa leo, Kushoto ni Uncle Jimmy Temu na Kulia ni Blogger Victor 
 Ndani ya Praise Power tuikuwa na Double E Sisters hapa liliachiliwa Sebene la Ukweli.
 Uncle Jimmy ya Victor wakichambya mambo ya Viva Shusho Viva Tanzania
 Double E Sisters ndani ya Praise Power Fm
Wametokezeleaje??

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...