15 June 2012


Friday, 15 June 2012

MUNGU NI MWEMA KWANGU--ANENA MDOGO WAKE ANGELO BUENAVISTA WA TAMTHILIA YA THE PROMISE

Jodi Santamaria a.k.a Lia Buenavista.

''Ninafuraha sana kwa baraka ambazo Mungu amekuwa akinijalia maishani mwangu, Mungu amekuwa mwema kwangu,hakika ni mwema wakati wote'', hayo ni maneno ya mwigizaji wa nchini Ufilipino mwanadada Jodi Santamaria ambaye hapa nchini anafahamika zaidi kwa jina la Lia baada ya kuigiza kwenye tamthilia iliyojipatia umaarufu nchini ya The Promise akiigiza kama mtoto wa madam Claudia na Eduardo Buenavista ama mdogo wake na Angelo.
Mwigizaji huyu amezungumza hayo wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Buzz cha nchini kwao Ufilipino kuhusiana na kuigiza tamthilia mpya hivi karibuni ''I’m really happy with all the blessings na dumarating. God has been really good to me. He's good all the time'', amesema Jodi ambaye aliachana na mumewe bwana Pampi Lacson miaka miwili iliyopita kutokana na matatizo yao ambayo hawakutaka kuyazungumza hadharani ambapo kwasasa mwanaume huyo anadaiwa kuanzisha uhusiano na msichana anayejihusisha na mambo ya urembo aitwaye Iwa Moto, ingawa kwa upande wake Jodi hataki kuzungumza lolote zaidi ya kubaki na Mungu wake pamoja na kumlea mtoto wake.
Jodi akiwa na mumewe Pampi Lacson pamoja na mtoto wao Thirdy.
                         
Mwigizaji huyo ambaye anatarajia kutimiza miaka 29 ya kuzaliwa hapo kesho, amesema angependa kufanya sherehe ndogo ambayo amesema itakuwa kama kuwashirikisha watu wengine baraka ambazo Mungu amekuwa akimjalia. Waigizaji nchini Ufilipino wengi wao wameonekana kumtanguliza Mungu mbele katika shughuli zao kwakumaanisha na wengine ikielezwa na mashabiki wa nchi hiyo kuwa wanazungumza kwa maneno tu na sio vitendo.

Kati ya wasanii ambao wamekuwa kioo kwa wengine kwasasa na wamekuwa wakipata sapoti ya maombi kutoka kwa mashabiki wenye kumuamini Mungu ni mwanadada Kristine Hermosa(Yna, Ara, Ella) pamoja na mumewe Oyo boy Sotto( Erick) aliyeigiza naye kwenye princess fish port zote zilionyeshwa na TBC wakati huo ikijulikana kama TVT,waigizaji hawa ambao Mungu amewajalia mtoto wa kike mwaka jana wakati wa Krismas pia wana mtoto mwingine wanayemlea baada ya kumchukua kutoka kwenye kituo cha watoto yatima, wamekuwa wakipata sapoti kubwa ya maombi na watu kupenda jinsi walivyowanyenyekevu katika maisha yao.

HAPA JIKUMBUSHE TAMTHILIA YA THE PROMISE KIPANDE AMBACHO UTAMUONA  JODI AKIIGIZA KATIKA TAMTHILIA HII (LUGHA KIFILIPINO)

Kristine na mumewe Oyo walipotoa picha za familia yao rasmi kwa mara ya kwanza kwa gazeti la

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...