20 June 2012

Kanisa lina Mengi ya kujifunza baada ya DNA kutangaza kurudi kufanya secular Music


DNA
Kwa afrika Mashariki na kati jina DNA(Denis Kagia) sio geni masikioni mwa wafuatiliaji wa muziki, DNA ni mwanamuziki kutoka nchini Kenya aliyetambulika na kupata sifa nyingi baada ya kutoa nyimbo yake ya BANJUKA,mwaka juzi DNA alitangaza kuwa ameokoka.Kwa waliokuwa wanamfatilia kwa kina utagundua DNA alisema wazi kuwa baada ya kuokoka anayafurahia maisha ya wokovu kwa kuwa yamemtenganisha na Pombe na sigara vitu ambavyo alishindwa kuachana navyo hadi alipookoka.Baada ya kuokoka DNA alianza kufanya muziki wa injili huku akifanya kazi ya utangazaji katika moja ya vituo vya redio vya kikrsto nchini Kenya.

Wiki iliyopita DNA akiongea na waandishi wa habari alitangaza rasmi kuwa ameamua kurudi na kufanya muziki wa DUNIA yaani aliokuwa akiufanya mwanzo kabla ya kuokoka na atabase kufanya all clubbing heats na tayari ameshafanya nyimbo mmoja iitwayo “Maswali ya Polisi”.Sehemu kubwa ya wakenya waimbaji na wafuatiliaji wa muziki wa injili nchini humo wameonekana kuuponda uamuzi huo na wengine kuubeza au kumbeza DNA mwenyewe.
Kwa Kanisa, suala la DNA linatoa uwanja mpana wa kujikagua na kujikumbusha kuwa wokovu ni NEEMA,leo DNA ameamua alichoamua na kanisa linasonga mbele sio kwa sababu mimi na wewe{Kanisa} ni wasafi sana kuliko yeye bali KWA NEEMA ya Bwana tunasonga mbele.

Kanisa linapozidi kukaa chini na kumhukumu DNA pasipo kumuombea huku ni kupoteza FOCUS ya safari yetu ya wokovu.Kwa kuwa kimsingi DNA sio wa kwanza kufanya hivyo na hatakuwa wa mwisho ila uamuzi wake unatupa wasaa wa kuangalia vitu gani ambavyo vinatusababisha wewe na mimi(kanisa) tuendelee na wokovu na kisha kuzidi kuvishikilia.
Kanisa halina budi kulichukulia suala la DNA kama darasa, na hapa ninamaanisha wapo wanamuziki wengi NGULI nchini na duniani ambao KRISTO atawaokoa,kuteleza kwa DNA kunatoa darasa huru katika kuwaelekeza hao Maceleb watakaookoka namna ya kudumu katika wokovu na nini wakiepuke ili wasirudi nyuma. Leo hii kuna namba kubwa ya maceleb waliookoka na mpaka leo wanaendelea na wokovu wakiwemo K-Basil,Renee Lamira,Chuck Norris (filamu),Cosmas Chidumule,Mzee Makasy,Mc Hummer,Stara Thomas na wengine wengi.

Mwisho ni vizuri Kanisa endapo litatumia muda mrefu katika kuwafundisha waongofu wapya namna ya kuliishia NENO na kudumu katika maombi, hii itasaidia katika kujenga internal strength ya mtu wakati anatoka na kujitangaza.Kwa uzoefu wangu nimegundua watu wengi maarufu ambao baada tu ya kuokoka na kukaa muda mfupi kwenye wokovu (i mean sio chini ya miaka miwili), wanapofanya kanisani kile walichokuwa wakikifanya huko duniani huwa hakina nguvu, na hii ni kwa kuwa vita yake ni kubwa kuliko nguvu ya Mungu aliyoiunda katika kulifanikisha hilo jambo      VICTOR-HOSSANAINC

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...