11 June 2012

Pastor Harris Kapiga Ashusha Sindano 7 kali za Moto kwenye Kitchen Party Gala.

Ni ugahamu wa Ajabu Sana Kuwa Kitchen Party kufundishana Wanawake kwa Wanawake, Kama ingekuwa mawazo yangu Kitchen Party Ingekuwa inafunzwa na wanaume. Kuna mambo ambayo Wanaume tunajua kwa Ujumla wetu na hayo yakiwa applied asilimia kubwa ya wanaume Wanakamatika.


Ugonjwa wa Suzuki Ukipelekwa Kampuni ya Corolla unaweza usitibike sawa sawa, ila Corolla peleka Corolla, ukitaka kujua Kwanini Wanaume wa siku hizi hawatulii Waulize wanaume usiulize Wanawake.

Mchungaji, Mtangazaji na MC maarufu Mjini Harris Kapiga ameshusha Sindano 7 kali za Moto kwa Wakina dada wa Jiji la Dar-es-Salaama pale alipokuwa akiongea kwenye Kitchen Party Gala inayoandaliwa na Mtangazaji Maarufu wa Clouds FM, Bibie Dina Marios.

Akizungumza katika Jioni hiyo ya tarehe 9 June, 2012 Pastor Harris alisema "Engine Kubwa ya Kudumisha Mapenzi kwa Wanaume hasa walio katika Ndoa, ni Creativity"

Kanisa limeanza kupewa nafasi katika Secular issues baada ya kuonekana Kanisa Lina majibu ya Mambo mengi yanayokosa majibu nje ya kanisa. Mnenaji mwingine katika Event hiyo alikuwa Pastor Fredy Kyala.

Big Up Kwa Kaka Mkubwa Harris Kapiga.



Pastor Harris Kapiga a.k.a HK One akishusha Sindano Ya 6 kwenye Kitchen Party Gala

Khaa Hapa kumbe Hajavaa Pete, Baba Larry vipi bwana.

Hawa wakitabasamu kufuatia sindano 7 za Pastor Kapiga.

Clouds Fm Tema huku Dina Marios huku Harris Kapiga.
Msemaji wa kutoka kiumeni Frederick Kyara...somo lilikuwa wanaume hawapendi nini ambavyo sisi wanawake tunavifanya kila siku mwisho wa siku ugomvi hauishi katika mahusiano.Hawapendi kuambiwa cha kufanya,hawapendi kuhisiwa hisiwa na kusachiwa sachiwa,kuamrishwa,kufananishwa mengi mengineyo vyote hivyo vilikuwa na maelezo na nini kifanyike?

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...