25 June 2012

Monday, June 25, 2012

Papaa Kumuwakilisha Christina Shusho Nchini Uingereza



Zikiwa zimebaki Siku 5 tu yaani tarehe 30 June, 2012 Ili kufikia tamati ya upigaji kura kwa ajili ya Kumuwezesha Mwanamuziki Pekee wa Kike Tanzania Christina Shusho kushinda katika Category mbili alizochaguliwa kuingia. Mwanamuziki huyo amefunguka katika Radio Ya Watu Clouds FM, na Kueleza kuwa Yamkini akatuma Mwakilishi siku ya Kugawiwa tuzo hizo siku ya tarehe 7 Mwezi 7, 2012 nchini Uingereza.


Christina Shusho Mwanamuziki Pekee wa Tanzania aliyechaguliwa kuingia katika Category 2. Zikiwa kama ifuatavyo.


1.  Mwanamuziki Bora Kutoka Africa Mashariki
2. Mwanamuziki Bora Wa Kike Barani Africa.
              Shusho Kushoto, Papaa Ze Blogger Katikati na Kulia ni Mtangazaji Pastor Harris Kapiga


akihojiwa na Mtangangazaji mahiri Pastor Harris Kapiga katika Kipindi cha Gospel Track  hivi karibuni kupitia Radio ya Clouds FM yenye kusikika ulimwengu Mzima Mwanamuziki huyo amefunguka na kusema, kutokana na Majukumu yanayomkabiri kwa sasa huenda akamtuma Mwakilishi ambaye ni Papaa Ze Blogger kwenda Kumuwakilisha katika Tuzo hizo katika nchi ya Uingereza.

Watanzania tunayo sababu ya Kumpigia Kura Mwanamuzi huyu wa Injili ili kuweza Kutwaa tuzo hizo 2.

Ili kuweza Kumpigia Kura Shusho Sasa hivi Bonyeza ...http://www.ballotbin.com/voterReg.php?b=29492

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...