31 March 2012


Saturday, March 31, 2012

The VOICE warekodi Live DvD Album



Usiku wa jana  kuanzia saa tatu usiku katika ukumbi wa Jumba la Makumbusho unaotazamana na chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) jijini Dar es salaam. Kundi maarufu la muziki wa injili liimbalo kwa mtindo wa Akapela lijulikanalo kama THE VOICE, lilikuwa likirekodi LIVE DVD Album. Kwa yeyote Yule aliyefika ukumbini hapo atakubaliana na Hosanna Inc kuwa vijana hawa wanavipaji vya tofauti katika kumtukuza Mungu.

Kundi hili linaloundwa na vijana watano ambao kati yao wanne wanatoka katika familia moja,lilianza kuimba nyimbo ya kwanza iliyopokelewa kwa shangwe ukumbini hapo iitwayo KWENYE MAVUNO, kisha wakaimba nyimbo yao maarufu NAJIVUNIA YESU WANGU ambayo waliimba kwa lafudhi ya Kimasai.Kabla The Voice hawajapanda jukwaani Mc wa shughuli hiyo Minister Godwin Gondwe, aliwakaribisha wageni wote waalikwa kisha shughuli akaanza.Hii ni moja kati ya Live DvD album ambayo ikitoka hutakiwi kuikosa.

The Voice wakiwasalimia mamia ya watu waliojitokeza ukumbini hapo
 Jembe!!!, hawa jamaa wako Vizuri,  ndivyo alivyokuwa akikiri Sam Papaa Katikati ya watu hapo  wakati shughuli ikiendelea.

The Voice wakiendelea kumtukuza Mungu ukumbini hapo

Sehemu ya Umati uliohudhuria tukio hilo

Kulia ni Kijana anaitwa Josiah ambaye ni pekee asiye kuwa ndugu wa damu katika kundi hilo,Huyu Mkaka anaimba sauti ya nne ipasavyo.

Live Recording Ikiendelea

Hapa The Voice wakiimba pamoja na mmoja wa wapiga-solo mahiri nchini Bro Sam Yonanyuma mwenye Gitaa


Kiongozi wa kundi la The VOICE Bro Obedi, akimtambulisha mama yao Mzazi(The First Lady of The Voice), kwa umati uliokuwepo ukumbini hapo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...