26 March 2012

Monday, March 26, 2012

Gospel Star Search Is Back.......

Mwishoni mwa Miaka ya 90 na Mwanzoni ya 2000, Wanamuziki Wa Injili wengi walianza kuibuka katika tasnia ya Gospel Music na kuwapiga kumbo wanamuziki 'Solo Artist" waliovuma sana kipindi cha Nyumba kama Mwl. Mwalubalile, Mzungu Four, Kyande, Munushi na Mwasumbi. Kati ya Wanamuziki hao walioibuka wengi waliibuliwa na mchakato mzima wa Gospel Star Search.

Nakumbuka Siku ya Fainali pale Diamond Jubilee, Mwanamuziki Jesca Honore alivyokamata watu kwa Wimbo wake wa Tenzi na mwisho kutunukiwa Zawadi ya gari kama mshindi wa Kwanza. Gospel Star Search iliwatambulisha kwenye Tasnia Wanamuziki Chipikizi kama Victor Aron, Amoke Kyando, Charles Mallya, Jonsia Ivatas, Raymond, Jesca Honore, Luiza, Angela Benard na wengine wengi ambao mpaka sasa wamekamata Anga la Muziki wa Injili.
    Baadhi ya Wajumbe wa Organizing Committee wa Gospel Star Search 2012-Kutoka Kushoto ni Papaa Ze Blogger, Anna Nelson, Michael Nkya, Harris Kapiga, Ikupa Ngao na Husdson Kamoga

Baada ya kuwa kimya Muda Mrefu Wale waaandaaji wa Tanzania Gospel Music Awards sasa wamekuja na Project ya "Gospel Star Search". Mwenyekiti wa Maandalizi hayo Mchungaji na Mtangazaji wa Clouds Redio Mr. Harris Kapiga (HK One) amefunguka na kuongea na Blog kuhusu mchakato huo.

Blogger: Kaka pole na Mujukumu ya Ibada na Weekend kwa Ujumla.

HK One: Namshukuru Mungu aisee, Weekend imekuwa Njema, Kwaresma ndo inaisha Isha hivyo.

Blogger : Kaka nimesikia tetesi kuwa Gospel Star Search imerudi tena kwa Next Level baada ya kuwa Kimya sana.

HK One: Kimya Kingi kina mshindo Mkuu, Ni Kweli Gospel Star Search imerudi tena na Safari hii imerudi Kimataifa Zaidi sababu haiko kama ile ya miaka iliyopita.
Hawa ni Kati walioshiriki Gospel Star Search ya kwanza miaka 7 iliyopita, Kutoka Kushoto ni Jesca Honore aliyeibuka mshindi, anayefuata ni Jonsia Ivatas ambaye kwa sasa ni Mama Mchungaji, Thobias ambaye mwaka jana alipata Tuzo za Mwanamuziki Bora wa Kiume katika Gospel Music Awards na Kulia ni Victor Aron.

Blogger: Hapo ni sawa, Lini unadhani Mchakato wa Kuwasaka na Kuibua vipaji vipya katika Gospel Music utaanza rasmi chini ya Brand "Gospel Star Search".

HK One: Mchakato rasmi unatazamia kuanza rasmi mwezi April na utatuchukua kama muda wa miezi mitatu ili kukamilisha zoezi la kupata Mfalme ama Malkia wa Gospel Music.

Blogger: Je Mchakato huu utashirikisha na mikoa mingine ama ni Dar-es-Salaam peke yake?

HK One: Mchakato huu utaanza kwa Kushirikisha Wilaya Zote Tatu za Mkoa wa Dar-es-Salaam ambapo tutaanzia Temeke, tutakuja Ilala na Mwisho kabisa ni Kinondoni.. Mbali na Dar-es-Salaam, tutaenda mikoani ambapo tumeigawa katika Kanda, baadhi ya kanda hizo ni Kanda ya Kati, Kanda ya Juu Kusini, Kanda ya Ziwa na kanda ya Kaskazini.
Kushoto ni Anna Nelson ambaye ni Mtangazaji wa Tv ya Trenet na Kulia ni Michael Nkya ambaye alikuwa mwalimu wa Kambi iliyopita ya Gospel Star Search

Blogger: Ninaamini katika Gospel wengi watajitokeza kushindania nafasi hizo, je Utaratibu wa Kushiriki Umekaaje?

HK One: Mpaka sasa utaratibu ni kwamba Matangazo yatatolewa na watu wataalikwa na washiriki watapewa namba kwa ajili ya kushiriki katika ushindani huo. Na katika Mchakato huu hatuna Kikomo cha Umri yeyote anayetaka kushiriki basi atakaribishwa.

Blogger: Kuna Ushirikishwaji wa Wadau wengine wa Muziki wa Injili?ama ni kikundi cha watu wachache.\

HK One: Ushirikishwaji Umezingatiwa mfano katika Mikoa shiriki mawasiliano bado yanafanyika ya Wadau wa Muziki wa Injili katika Mikoa hiyo. Na hata "Ma-Judge" ni watu wenye Upeo Mkubwa wa Mambo ya Muziki wa Injili lakini pia wenye Kumjua Mungu Vizuri.

Blogger: Ninawatakia Matayarisho mema na tutakuwa bega kwa bega katika "kufunguka" kwenye jamii.

HK One. Asante Kaka Tukutane tena kwa taarifa zaidi.

Blog Itakuwa inakupa Updates Kila Iitwapo leo, Stay Tune With Ze Blogger.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...