08 April 2013


Tamasha La Pasaka La Konga Nyoyo ndani ya Jiji la Dar-es-Salaam

Pamoja na Mvua Kubwa iliyonyesha leo katika jiji la Dar-es-Salaam Maelfu Ya Wakazi wa Jiji la Dar wamejitokeza katika Tamasha la Pasaka lililofanyika katika Uwanja wa Taifa.

Tamasha Pasaka ni Tamasha linalofanyika Kila Mwaka mara moja katika Msimu wa Pasaka ambapo wanamuziki wa nje na ndani ya Tanzania wanakuwa na muda wa pamoja wa Kusifu na Kumwabudu Mungu.

Mwaka 2013 Kauli Mbiu ya Tamasha ni Amani na Utulivu ambapo fedha zitakazopatikana ni maalum kwa ajili ya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Katika siku ya leo Mgeni rasmi alikuwa ni Mhe. Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye mara kadhaa alipata shuruba ya kupigiwa makelele mara kwa mara kutokana na kukatika katika kwa umeme mara kwa mara.

Mwanamuzi Mwalikwa wa Mwaka huu Kutoka Africa ya Kusini ni Sipho Makabane ambaye jioni ya leo amefanya Performance ya nyimbo 10 Mfululizo ndani ya uwanja huo na Kukonga nyoyo za watu waliohudhuria Tamasha la leo. Malkia wa Muziki wa Injili Tanzania Rose Muhando alifanya kile ambacho kilitarajiwa na Wakazi wa Jiji kwa Kuimba wimbo wa Utamu wa Yesu ulioombwa na Mhe. Mgeni rasmi.

Wanamuziki Wengine waliokuwepo siku ya leo ni Christ Ambassadors kutoka Rwanda, Solomon Mukubwa, Anastazia Mukabwa, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, John Lisu, Faraja Mtabobwa na Glorious Worship Team.
Waimbaji Wa Christ Ambassadors kutoka Rwanda walishuka Kutoka Jukwaani na kugusa wanakazi wa jiji la dar na wimbo wao "Kwetu Pazuri" 

Mwanamuziki Wa Injili wa Tanzania Upendo Kilahiro akienda sawa Siku Ya Leo

Upendo Nkone akiwa Jukwaaani
Anastazia Mukabwa kutoka Kenya akiwa na Rose Muhando ambao kwa pamoja wameimba wimbo wa "Kiatu Kivue"
 Christ Ambassadors Choir wakiwa tayari kwa ajili ya Kazi. 
Solomoni Mukubwa akiwa anapadna Stejini tayari kwa ajili ya Kuimba siku ya leo

Ephrahim Sekeleti Mwuimbaji Kutoka Zambia akiwa George Mpella na Hudson Kamoga
Glorious Worship Team wakienda Sawa siku Ya Leo
Malkia wa Muziki wa Injili Rose Muhando akiwa Kikazi Zaidi

Ephrahim Sekeleti akienda Sawa Siku Ya leo
Sipho Makabane akiwa kikazi Zaidi siku Ya leo
Sehemu Ya Umati Wa Watu

Rose akiendelea na Kazi huku Waandishi na Walinzi wakiwa wamemzunguka
Sipho akijiandaa kuingia Jukwaani
Pole Pole akisogelea Umati Wa watu
Koti Likawa Zito
Kikazi Zaidi
Hapa wakitengeneza Tangazo la Chomoza
Bon Mwaitege akiwa mbele ya Camera Man Ray wa Clouds Tv.
Sipho akienda Sawa na Wananchi siku ya leo
Watu Nyomiiiii
Wakati Sipho akiimba ni kama ilikuwa Mchaka Mchaka Kulia ni Anastazia, Rose Muhando Upendo Nkone na Solomon wakimpa Support Sipho.
John  Lisu 

Without Caption 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...