17 April 2013

MAZISHI YA WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA UINGEREZA MARGRET THATCHER YAFANYIKA MJINI LONDON

Jeneza la Margaret Thatcher 
VIONGOZI na watu maarufu katika nchi 170 kote duniani wako mjini London kuhudhuria mazishi ya waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Margret Thatcher maarufu kama Iron Lady. 
Maelfu ya watu mjini London wamepiga kambi tangu usiku wa wa kuamkia leo katika kanisa katoliki la St. Paul, kuliona jeneza la Margret Thatcher lililofinikwa kwa bendera ya Uingereza, shada kubwa la maua juu yake na kusindikizwa na jeshi la nchi hiyo.
Waombolezaji katika mazishi ya Margaret Thatcher 
  Waombolezaji katika mazishi ya Margaret Thatcher.
 
Anthony Boutall mkaazi wa London aliye na umri wa miaka 25 amesema ameamka na kufika nje ya kanisa hilo kushuhudia mazishi ya shujaa ambaye aliibeba na kuinua Uingereza. 

Bendera kote nchini humo zimepeperushwa nusu mlingoti kutoa heshima kwa mwendazake Margret Thatcher aliyekuwa akiugua kiharusi na kufariki tarehe 8 mwezi huu akiwa na umri wa miaka 87.

Sio wote wanaoomboleza kifo cha Thatcher
Hata hivyo sio wote nchini Uingereza wanaoomboleza kifo cha bibi wa Chuma-Iron Lady, Mamia ya wapinzani wa kisiasa wamesema watanyamaa kimya kwa dakika moja na kulipa mgongo jeneza hilo litakapopitishwa.
Waandamanaji katika mazishi ya Thatcher 
  Waandamanaji katika mazishi ya Thatcher.
 
Kwa upande wake Henry Page amabye ni mwalimu msataafu aliyebeba bango lililopinga mamilioni ya fedha yaliotumika kuandaa mazishi ya Thatcher, amesema gharama ya juu haipaswi kutumika katika mazishi ya mtu ambaye katika uongozi wake aliwagawanya waingereza katika misingi ya kijamii na hata kiuchumi.
Takriban dola milioni 15 zimetumika katika mazishi hayo.

Jeneza la Margret Thatcher kwa sasa linapitishwa kutoka katika majengo ya bunge, kupelekwa katika kanisa la St. Clement Danes, kisha kuwekwa katika msafara wa farasi na kuanza kusafirishwa tena pole pole hadi katika kanisa katoliki la St Paul ambako wageni waalikwa takriban 2300 akiwemo Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza watakuwepo kupokea mwili huo.

Usalama waimarishwa.
Polisi takriban 4000 wamesambazwa kote mjini humo kuimarisha usalama. Kiongozi huyo wa zamani ambaye alipewa jina hilo la Bibi wa Chuma- Iron Lady aliibadilisha Uingereza katika kipindi cha miaka 11 alichoongoza kama waziri mkuu wa nchi hiyo kuanzia mwaka wa 1979 hadi 1990.
Usalama waimarishwa  
  Usalama waimarishwa.
 
Wanaohudhuria mazishi ya Thatcher ni pamoja na Malkia Elizabeth wa Uingereza, mumewe Prince Philip, Mawaziri wakuu 11 kutoka mataifa mbali mbali duniani, waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani Henry Kissinger na makamu wa zamani wa rais wa Marekani Dick Cheney.

Wageni maarufu waliotoa udhuru wa kutohudhuria mazishi hayo ni kiongozi wa zamani wa kisovieti Mikhail Gorbachev na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel atawakilishwa waziri wake wa mambo ya nje.

Hata hivyo familia ya Bill Clinton na George Bush zilikataa kuhudhuria mazishi hayo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...