12 February 2013

John Lisu Aachilia Rasmi "Uko Hapa" Ndani Ya CCC

Mwanamuziki Wa Injili Tanzania anayepiga Muziki wa Live, John Lisu Leo amezindua albam yake ya Pili yenye Jina la "Uko Hapa" Mwanamuzi Huyo ambaye alifanya uzinduzi katika Kanisa Maarufu la CCC na Kuhuduriwa na maelfu ya Wakazi wa Jiji la Dar.

Uzinduzi huo uliosindikizwa na Wanamuziki wengine wa Injili kama Cosmas Chidumule, The Voice, Pastor Safari, Glorious Celebration na Next Level lilikuwa ni Tamasha la Aina yake.

John Lisu akiongea na Blog anasema "anamshukuru Mungu kwa idadi ya watu waliojitokeza, anamshukuru Mungu pia kwa uwepo wake uliowagusa watu katika Uzinduzi huo.

John Lisu amezindua albam yake ya pili ya audio yenye jumla ya nyimbo 11 na itaanza kupatikana kuanzia siku ya leo.
 Mdau wa Blog Hii Pascal akiwa na Mkewe Dativa wakiwa ndani ya Ukumbi wa CCC
 Kwa Mbaliiii
 Bishop Dr. Ranwell Mwenisongole akifungua rasmi tamasha hilo
 Swahiba akiwa mbele ya Mojawapo wa Kazi zake alizomfanyia Lisu, Prosper Mwakitalima ndiye aliye Print Tshirt, Banners na Tickets, Pia ndiye aliye buni.
 Daniel akiwa na Amani wakienda Sawa
 Music Director, Sam Yona
 Waimbaji Wakienda Sawa
 John Lisu akiongoza Kikosi kwa ajili ya Kazi
 Habari Ndo Hii
 Waimbaji Wa John Lisu wakienda sawa
 Watu wakienda sawa
Mke Wa John Lisu akipiga mojawapo ya nyimbo leo jioni.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...