11 May 2013


BREAKING NEWS : MWIMBAJI NYOTA WA GOSPEL APATA AJALI USIKU HUU


Habari ambazo GK imezipata muda mfupi uliopita kutoka nchini Afrika ya kusini, inadaiwa kuwa mwanamuziki nyota wa muziki wa injili nchini humo Kgotso Makgalema amepata ajali ya gari usiku wa leo wakati akielekea eneo la Bloemfontein nchini humo.

Baadhi ya mashabiki wa mwimbaji huyo waliopata ujumbe huo wametuma meseji mbalimbali katika ukurasa wake wa Facebook za kumtakia uponyaji mwimbaji huyo, huku ikionyesha kwamba mwimbaji huyo yuko kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) *ingawa hata hivyo bado haijatangazwa rasmi. GK itakupa taarifa kamili pindi tutakapozipata.





  • Im praying for u Kgotso..wishing u a speedy recorvery....God will make His way for u cos His mercy is ever lasting.. — with Kgotso Makgalema.
  • ICU- Its God wu says, I See You, u r nt in danger, u r broken bt u r stil in da hand, God wl remake u again, its nt ova until God says its ova. B wel man of God.
  • We are praying with you man of God.You have a long way with God. Jesus & the whole heaven is fighting for you right now in Jesus mighty name. We are praying for you.
  • All is well KAKAPA...God is with you bra..
  • My prayers r with u...be strong in de lord u are a fighter.



  • Wakati huohuo Ntokozo Mbambo wa Nqubeko ameibuka na tuzo ya album bora ya muziki wa injili kupitia tuzo kubwa za muziki nchini humo ziitwazo South African Music Awards ambazo zimefanyika kwa mara ya 19 usiku wa leo, ukiacha Ntokozo pia kundi la Joyous Celebration limeondoka na tuzo ya album bora inayoongoza kwa kuuza nakala nyingi nchini humo, kupitia album yake ya 16 huku kijana Khaya Mthethwa mshindi wa South African Idol na mwimbaji wa Joyous naye pia kaondoka na tuzo usiku wa leo.

    No comments:

    Post a Comment

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...