08 February 2013

Jesca Honore Kuvunja Ukimya na Albam ya "Nimevunja Ukimya"

Mwanamuziki Mahiri wa Injili aliyejitoa kutoka Kundi la Glorious Celebration ameiambia blog kuwa anatarajia kufanya mambo makubwa 2013 katika tasnia ya Muziki wa Injili hata Tanzania. Mwanamuziki huyu ame-efatha mbele ya Blogger na kueleza mipango yake ya 2013 lakini pia akieleza kuwa Mwezi May Mwaka huu anatarajia kufunga pingu za Maisha na Mtangazaji wa Kituo Cha Tv hapa Tanzania.

Katika kueleza Mipango yake Mwanamuziki Jesca Honore ameeleza kuwa mwezi March, 2013 tarehe 10 anatarajia kufanya Preview Ya Vision yake katika Muziki wa Injili lakini Pia Kuzindua Eneo la Serena Hotel kama sehemu ambayo atakuwa akifanya Muziki Wa Injili Kila Ijumaa sehemu hiyo.

Akizungumza na Blog Hii Jesca Honore amesema anatarajia kuzindua albam yenye jina la "Nimevunja Ukimya" ulio katika mahadhi ya Kwaito na Katika Uzinduzi huo Utakaofanyika Serena Hotel Utaambatana na Preview ya Vision Ya Jesca Honore. Albam hiyo yenye mchanganyiko wa Mahadhi mbalimbali imefanywa katika Viwango Vya Kimataifa.


Mungu akutumie katika huduma yako mpya!!!Hapa Glorious Celebration tunakutakia Mema....md

07 February 2013

7,2, 2013

Mpiga Drums Nambari One Wa Joyous Celebration Ajitoa



Mwaka Jana Mapema kabisa Wanamuziki Maarufu Mume na Mke walijitoa katika Kundi Maarufu la JC mwaka huu majira yale yale Mpiga drums nambari wa Joyous Celebration mwenye jina la Siyabulela Satsha ametangaza Kujitoa katika kundi hilo na baada ya Mkataba wake Kumalizika.


Joyous Celebration imekwisha kutoa nafasi ya Kazi ya Jembe hilo ambalo taarifa za Awali zinasema anakwenda kufanya kazi pamoja na Wanamuziki wengine waliokuwa katika kundi hilo na Kujiondoa mapema mwaka jana.


Kumekuwa na mapendekezo kadhaa ya dogo aliyeonekana katika JC 15 miaka miwili iliyopita kuziba gap la mpiga drums huyo. Oyanda ambaye amekuwa akifanya mazoezi na JC kwa muda mrefu ambaye pia ni mmoja wa wanaosadikika kuchukua fomu kwa ajili ya nafasi hiyo anapewa nafasi kubwa zaidi ya kuwa mbeba mikoba hiyo. Changamoto kubwa ni umri alionao Mwanamuziki huo ambapo kwa sasa anamiaka 12-13 na bado yuko shuleni.


NABII FLORAH MTUMISHI WA MUNGU!

03 November 2012


Friday, November 2, 2012

Mungu Asipokujibu Maombi Yako Muulize Ni Kwa Nini Hajakujibu



SABABU NYINGI AMBAZO MUNGU HAJIBU MAOMBI
ZIPO NYINGI LAKINI NAKUONYESHA AMBAZO NI ADIMU

Mwl. Christopher Mwakasege

1.     KUTAKA KUJIBIWA MAOMBI YAKO NJE YA NJOZI AU NJE YA MAONO YA MUNGU
Habakuki 2: 1 – 3 … Bwana akanijibu, akasema iandike njozi hii  ukaifanye kuwa wazi sana katika …
  • Wakati Habakuki anaomba ondoa uovu/ udhalimu/ haki imepotoka, Mungu amenyamaza, halafu anaenda kuomba kwa nini Mungu hakujibu malalamiko yake ndipo Mungu akajibu!
  • Mungu hakujibu kutatua malalamiko yake ila Mungu alijibu malalamiko yake (Vs. 2 - 3)
Lile neno njozi kwa kiingereza limeandikwa vision na kwa Kiswahili lingefaa kuwa maono.
  • Mungu alikuwa anamwambia Habakuki badilisha aina ya uombaji wako,usiombe kwa kuangalia mazingira yanavyoonekana ila omba kwa kuangalia njozi
NJOZI za aina 3:
a). Njozi yake mwenyewe
b). Njozi ya eneo ambalo analiombea
c). Njozi ya maeneo ambayo habakuki alikuwa ana mazoea ya kukaa au kupita
Habakuki alikuwa anaelewa Mungu alikuwa na maana gani maana hakuna alipomwambia aina gani ya njozi aliandike!
Ndani ya hiyo mistari miwili yapo mambo 7 ambayo sitayataja hapa ila nitayataja kesho, leo  acha nieleze kidogo juu ya njozi/maono / vision. Maana kila mtu hapa atatoa tafsiri yake

MAANA YA NJOZI/ MAONO/ VISION
NJOZI/ MAONO/ VISION NI KUSUDI LA MUNGU LINALOFUNULIWA NDANI YA MTU KWA NJIA YA MFUMO WA PICHA, ni kusudi la Mungu linalowekwa ndani yako linapofunuliwa linakuwa maono/ vision.
Na linapofunuliwa linakupa kuona angalau vitu 3 au kimoja wapo au vyote vitatu kwa pamoja:

1. Kukupa sababu ya kuumbwa kwa kitu/ kuwepo kwa kitu,
Sababu ya kuwepo kampuni/ nchi / ndoa, cho chote kile na unapopewa sababu na ikifunuliwa ndani yako ile sababu inakuwa vision.
Bangi ni mbaya kwa sababu hatujui makusudi ya Mungu kuiumba. Hivyo serikali imepewa na Mungu kuweka sheria ya kuhakikisha kuwa bangi haitumiki vibaya mpaka pale tutakapojua matumizi mazuri ya bangi.
Ajali nyingi za mabasi ni kwa sababu ya utengenezaji wa mabasi, mabasi yana chases yake na magari ya kubeba mizigo yana chases. Unakuta mtu ananunua kichwa cha lorry na anachonga basi, ukilitazama kwa nje unaona linapendeza na linapokimbizwa na kukata kona gari linamshinda dereva kwa sababu halikuundiwa kukata kona likiwa na watu lakini likiwa na mizigo halafu tunasema ni shetani.


2. Kukupa picha ya mwishoni wa jambo ukiwa mwanzoni, maono yanakupa mwisho wa jambo ukiwa mwanzoni mwake. Na unapoona mwisho wake unapata ndani yako msukumo, na mtu asiyeona mwisho wa jambo anaweza kukatishwa tamaa maana hajaona mwisho wake lakini yule aliyeona mwisho wake hauwezi kumkatisha tamaa hata iweje!
Kabla nyumba haijawa nyuma inakuwa nyumba ndani ya mtu. Mchoraji anaweza kuweka kwenye computer na anaonyesha kilichondani yake na hata ukimwambia kuwa hii nyumba haiwezi kujingwa hawezi kukuelewa kwa sababu hameiona

3. Kusudi la Mungu linakupa ‘motive’ (kujua)
Wakati wa kesi za mauaji mahakamani wanachunguza sababu za kuua, i.e wakati hukumu inatolewa wanaangalia sababu ya kuuna na inapokuja kuwa aliua pasipo kukusudia adhabu yake ni tofauti. Kusudi la Mungu kukupa maoni ni kukupa kujua sababu ya kuwepo

WATU WENGI SANA WANACHANGANYA KATI YA WITO NA MAONO

Waefeso 4: 11 – 16  … mitume/ manabii/ waalimu/ wachungaji … KWA KUSUDI LAKE
Unamuuliza mtu wito wake anaeleza maono yake!
  • Kuitwa kuwa nabii, mtume, mwalimu hilo sio KUSUDI ni WITO
  • 2Timotheo 1: 8 – 9 … akatuita kwa mwito mtakatifu … KWA KADRI YA MAKUSUDI YAKE YEYE.
  • USIPOJUA KUSUDI LAKE HUTAJUA MAONO YAKO
  • Mungu aliponiita kuwa mwalimu anakusudi la kuniita kuwa mwalimu.
  • Unapoombea uinjilisti/ uchungani unaombea wito lakini hujaombea MAONO/ KUSUDI LA MUNGU
  • Mungu hawezi kukupa nje ya maono/ kusudi la kukuitia, ukiwa unaomba mkumbushe Mungu ndani ya maono/kusudi alilokuitia na mengine yote atakutimizia. Fedha hazijawa connected na maono! Mungu anakupa pesa kama una maono ya ile pesa/ huduma.
  • Mungu hawezi kumlipa mtu kwa kazi ya hasara
  • Wachungaji wanapata hali ngumu kifedha kwa sababu wanadhani wito ni maono na wanataka Mungu  awape pesa kwa ajili ya wito wakati Mungu anataka atoe pesa kwa ajili ya MAONO

Matendo 13: 36  … akiisha kutumikia SHAURI/KUSUDI LA BWANA…
Si kusudi la Israel/ kusudi la baba yake/ si kusudi la serikali ila KUSUDI LA MUNGU i.e alijua kusudi la Mungu.
  • Kampuni inaweza kuwepo na ukatumikia wito ukasahau kutumikia kusudi la Mungu

Kutoka 25: 1 – 9  … wamjengee HEMA ambalo Mungu atakaa ndani!
  • Kazi ya hema sio kukaliwa na watu ila Mungu
  • 2Samweli 7: 1 – 5 hekalu sio nyumba ya ibada ila NYUMBA YA MUNGU; Kwa sababu Mungu yupo ndani ndio maana ibada inafanyika – kama Mungu hayupo ndani ibada inafanyika ya nini?
  • Ukiacha kufuata kusudi la Mungu usithubutu kuulizia ulinzi wa kusudi la Mungu
  • Mtu aliye ndani ya kusudi na aliye nje ya kusudi wanapata vita vilivyosawa lakini ulinzi unatofautiana

 Mwl. Christopher Mwakasege

Friday, November 2, 2012

Mungu Asipokujibu Maombi Yako Muulize Ni Kwa Nini Hajakujibu



SABABU NYINGI AMBAZO MUNGU HAJIBU MAOMBI
ZIPO NYINGI LAKINI NAKUONYESHA AMBAZO NI ADIMU

Mwl. Christopher Mwakasege

1.     KUTAKA KUJIBIWA MAOMBI YAKO NJE YA NJOZI AU NJE YA MAONO YA MUNGU
Habakuki 2: 1 – 3 … Bwana akanijibu, akasema iandike njozi hii  ukaifanye kuwa wazi sana katika …
  • Wakati Habakuki anaomba ondoa uovu/ udhalimu/ haki imepotoka, Mungu amenyamaza, halafu anaenda kuomba kwa nini Mungu hakujibu malalamiko yake ndipo Mungu akajibu!
  • Mungu hakujibu kutatua malalamiko yake ila Mungu alijibu malalamiko yake (Vs. 2 - 3)
Lile neno njozi kwa kiingereza limeandikwa vision na kwa Kiswahili lingefaa kuwa maono.
  • Mungu alikuwa anamwambia Habakuki badilisha aina ya uombaji wako,usiombe kwa kuangalia mazingira yanavyoonekana ila omba kwa kuangalia njozi
NJOZI za aina 3:
a). Njozi yake mwenyewe
b). Njozi ya eneo ambalo analiombea
c). Njozi ya maeneo ambayo habakuki alikuwa ana mazoea ya kukaa au kupita
Habakuki alikuwa anaelewa Mungu alikuwa na maana gani maana hakuna alipomwambia aina gani ya njozi aliandike!
Ndani ya hiyo mistari miwili yapo mambo 7 ambayo sitayataja hapa ila nitayataja kesho, leo  acha nieleze kidogo juu ya njozi/maono / vision. Maana kila mtu hapa atatoa tafsiri yake

MAANA YA NJOZI/ MAONO/ VISION
NJOZI/ MAONO/ VISION NI KUSUDI LA MUNGU LINALOFUNULIWA NDANI YA MTU KWA NJIA YA MFUMO WA PICHA, ni kusudi la Mungu linalowekwa ndani yako linapofunuliwa linakuwa maono/ vision.
Na linapofunuliwa linakupa kuona angalau vitu 3 au kimoja wapo au vyote vitatu kwa pamoja:

1. Kukupa sababu ya kuumbwa kwa kitu/ kuwepo kwa kitu,
Sababu ya kuwepo kampuni/ nchi / ndoa, cho chote kile na unapopewa sababu na ikifunuliwa ndani yako ile sababu inakuwa vision.
Bangi ni mbaya kwa sababu hatujui makusudi ya Mungu kuiumba. Hivyo serikali imepewa na Mungu kuweka sheria ya kuhakikisha kuwa bangi haitumiki vibaya mpaka pale tutakapojua matumizi mazuri ya bangi.
Ajali nyingi za mabasi ni kwa sababu ya utengenezaji wa mabasi, mabasi yana chases yake na magari ya kubeba mizigo yana chases. Unakuta mtu ananunua kichwa cha lorry na anachonga basi, ukilitazama kwa nje unaona linapendeza na linapokimbizwa na kukata kona gari linamshinda dereva kwa sababu halikuundiwa kukata kona likiwa na watu lakini likiwa na mizigo halafu tunasema ni shetani.


2. Kukupa picha ya mwishoni wa jambo ukiwa mwanzoni, maono yanakupa mwisho wa jambo ukiwa mwanzoni mwake. Na unapoona mwisho wake unapata ndani yako msukumo, na mtu asiyeona mwisho wa jambo anaweza kukatishwa tamaa maana hajaona mwisho wake lakini yule aliyeona mwisho wake hauwezi kumkatisha tamaa hata iweje!
Kabla nyumba haijawa nyuma inakuwa nyumba ndani ya mtu. Mchoraji anaweza kuweka kwenye computer na anaonyesha kilichondani yake na hata ukimwambia kuwa hii nyumba haiwezi kujingwa hawezi kukuelewa kwa sababu hameiona

3. Kusudi la Mungu linakupa ‘motive’ (kujua)
Wakati wa kesi za mauaji mahakamani wanachunguza sababu za kuua, i.e wakati hukumu inatolewa wanaangalia sababu ya kuuna na inapokuja kuwa aliua pasipo kukusudia adhabu yake ni tofauti. Kusudi la Mungu kukupa maoni ni kukupa kujua sababu ya kuwepo

WATU WENGI SANA WANACHANGANYA KATI YA WITO NA MAONO

Waefeso 4: 11 – 16  … mitume/ manabii/ waalimu/ wachungaji … KWA KUSUDI LAKE
Unamuuliza mtu wito wake anaeleza maono yake!
  • Kuitwa kuwa nabii, mtume, mwalimu hilo sio KUSUDI ni WITO
  • 2Timotheo 1: 8 – 9 … akatuita kwa mwito mtakatifu … KWA KADRI YA MAKUSUDI YAKE YEYE.
  • USIPOJUA KUSUDI LAKE HUTAJUA MAONO YAKO
  • Mungu aliponiita kuwa mwalimu anakusudi la kuniita kuwa mwalimu.
  • Unapoombea uinjilisti/ uchungani unaombea wito lakini hujaombea MAONO/ KUSUDI LA MUNGU
  • Mungu hawezi kukupa nje ya maono/ kusudi la kukuitia, ukiwa unaomba mkumbushe Mungu ndani ya maono/kusudi alilokuitia na mengine yote atakutimizia. Fedha hazijawa connected na maono! Mungu anakupa pesa kama una maono ya ile pesa/ huduma.
  • Mungu hawezi kumlipa mtu kwa kazi ya hasara
  • Wachungaji wanapata hali ngumu kifedha kwa sababu wanadhani wito ni maono na wanataka Mungu  awape pesa kwa ajili ya wito wakati Mungu anataka atoe pesa kwa ajili ya MAONO

Matendo 13: 36  … akiisha kutumikia SHAURI/KUSUDI LA BWANA…
Si kusudi la Israel/ kusudi la baba yake/ si kusudi la serikali ila KUSUDI LA MUNGU i.e alijua kusudi la Mungu.
  • Kampuni inaweza kuwepo na ukatumikia wito ukasahau kutumikia kusudi la Mungu

Kutoka 25: 1 – 9  … wamjengee HEMA ambalo Mungu atakaa ndani!
  • Kazi ya hema sio kukaliwa na watu ila Mungu
  • 2Samweli 7: 1 – 5 hekalu sio nyumba ya ibada ila NYUMBA YA MUNGU; Kwa sababu Mungu yupo ndani ndio maana ibada inafanyika – kama Mungu hayupo ndani ibada inafanyika ya nini?
  • Ukiacha kufuata kusudi la Mungu usithubutu kuulizia ulinzi wa kusudi la Mungu
  • Mtu aliye ndani ya kusudi na aliye nje ya kusudi wanapata vita vilivyosawa lakini ulinzi unatofautiana

 Mwl. Christopher Mwakasege

05 August 2012

Launching Ya Let It Rain Ya Sara Shilla Next Level


Siku Ya Leo Katika Ukumbi wa Banora Maeneo Ya Survey Karibu na eneo la Mlimani City Mwanamuziki Wa Injili Sarah Shilla amezindua Albam Yake ya Kwanza yenye jina la “Let It Rain”.
 Mwenge Praise Team wakihudumu Siku Ya Leo
 Rivers Of Life Kutoka DPC chini Ya Pastor Safari Wakihudumu Siku Ya leo
Eunice akiwa na Kundi Lake
Katika Uzinduzi Huo Uliopambwa na vikundi mbalimbali vya uimbaji ulifana kwa aina yake katika Ukumbi huo wa Kisasa kabisa Jioni ya leo. Kati Ya Vikundi vilivyo hudumu siku ya leo ni Mwenge TAG Praise Team ambao waliongoza Kusifu na Kuabudu, wengine ni Rivers Of Life Wa DPC, Rivers Of Joy Wa VCC, Eunice and Miriam Lukindo Wa Mauki na wengine wengi
 Miriam Lukindo wa Mauki ndani ya Banora
Rivers Of Joy Kutoka VCC wakiwa Ndani ya Kumsindikiza Sarah Shilla Kwenye Launching ya albam. 

Mshehereshaji Mashuhuri jijini Dar, Mc King Chavalla ndiye aliyekuwa akiongoza shughuli nzima ya Jioni ya leo. Mbali na Kuongoza event hiyo pia Mc huyo alifanya Comedy kama ilivyo kawaida ya Mc huyo the King Of Stand Up Comedy.
 Mc wa Event King Chavala akiwa Kikazi Zaidi Siku Ya Leo
Pastor Safari Akifungua event ya Siku Ya leo.
Mwanamuziki wa Injili alipanda Jukwaani Majira ya Saa 12 jioni kwa style ya aina yake na kuhudumu nyimbo 5 mfululizo Jukwaani. Kisha Rev Dr. Huruma Nkone Alibariki Albam hiyo ya "Let It Rain In His Presence".
Rev. Dr. Huruma Nkone akiwa ndani ya Banora Siku Ya leo.

Blog Inatoa Big Up Kwa Sara Shila Kwa Siku ya leo Kufikia hatua hiyo.
 Watu Peopleeeeee Hand Uuuuuuuuuuup
 Papaa Ze Blogger Kama Kawa Akiwakilisha Siku Ya leo
 Without Caption Jana Na Leo....../....
 Sara Shilla Akihudumu Siku Ya Leo
 Tehe tehe Hawa Ndo Walibeba CD, Sijui Waliimba Baadae???
 Rev. Dr. Huruma Nkone akizindua Albam hiyo Siku Ya Leo Kwenye Ukumbi Wa Banora.

02 August 2012

Love Tanzania Festival kuyakutanisha zaidi ya Makanisa 800 nchini



Miwani 10,000 za kusomea kugawiwa Bure
Wafanyabiashara wakubwa na viongozi wa serikari kuinjilishwa kupitia Evening Dinner
Kikundi maalumu cha Michezo ya Baiskeli kuonyesha ufundi wa kuchezea baiskeli
Tofauti na Donnie Moen, Nicole C Mullen  ,Christina  Shusho,John Lissu,Pastor Safari Paul wa DPC kuongoza Love Tanzania Festival Praise Team

Love Tanzania Festival ni kusanyiko kubwa la kihistoria litakalofanyika kuanzia tarehe 11-12/08/2012 katika viwanja vya Jangwani kuanzia saa saba mchana mpaka saa 2 Usiku.Kwa mujibu wa mmoja wa waandaaji wa kusanyiko hilo Brother Prosper Mwakitalima ameiambia Hosanna Inc kuwa katika kufanikisha kusanyiko hilo makanisa zaidi ya 800 yameshiriki katika maandalizi ya tukio hilo maalumu lenye lengo la kuwakutanisha watu wa dini,kabila,rika zote kwa lengo la kumtukuza Kristo Yesu.

Kwa mujibu wa Mwakitalima kabla ya shughuli ya tarehe 11 na 12 kuna shughuli mbalimbali ambazo Love Tanzania Festival itakuwa ikizifanya kwa jamii ya Tanzania.

Ifuatayo ni Ratiba ya shughuli nzima za LOVE TANZANIA FESTIVAL.

Tarehe 5 August  7:00Asbh – 10.00 Asbh
Mbeba maono wa Love Tanzania Featival  mtumishi Andrew Palau atahubiri ibada zote mbili katika kanisa la Upanga City Christian Centre (UCC)

Muimbaji mashuhuri Nicole C Mullen atahudumu

Tarehe 7 August 10Asbh
Kutafanyika Mkutano wa waandishi wa habari(Press Confference) katika Ukumbi wa TBD ambapo Andrew Palau akiambatana na wachungaji, Maaskofu,waimbaji na kikundi cha waonyesha michezo ya Baiskeli watakuwa wakiongea na waandishi wa habari.
Usiku huo wa Tarehe 7 kuanzia saa 11.30 jioni katika ukumbi wa KARIMJEE  kutafanyika WOMENS DINNER ambapo kamati imewakaribisha zaidi ya wamama 600 nao watapata nafasi kusikiliza na ya kubadilishana mawazo na Andrew Palau.

Tarehe 8 August  12:00 jioni
Katika Ukumbi wa Karimjee Hall kutafanyika hafla ya chakula cha jioni ambapo viongozi mbalimbali wa serikali na wafanyabiashara wakubwa watapata nafasi ya kukutana na Palau ambapo mtumishi huyo atatumia nafasi hiyo kumtangaza kristo kwa tabaka hilo la watanzania ambao kwa namna moja au nyingine limekuwa ni vigumu kufikiwa na injili ya Yesu kristo.

Tarehe 10:August 8:00 Mchana – 9:00 Jioni
Kutafanyika maozoezi(Rehesal)ya michezo ya Baiskeli ambapo kikundi cha JUNGLE RUSH FMX  kutoka Afrika ya Kusini kitakuwa kikifanya mazoezi hayo ili kujiweka sawa.Baada ya mazoezi hayo kutafanyika MAOMBI rasmi kwa ajili ya kuuweka wakfu uwanja wa Jangwani kwa ajili ya shughuli nzima ya tarehe 11-12.



VITUO MAALUMU KWA AJILI YA CLINIC YA MACHO
Love Tanzania Festival siyo tu itahusisha kuponya ROHO za watu kupitia neno la Mungu, pia watakuwepo Madaktari maalumu wa macho kutoka Marekani na watashirikiana na madaktari wa ki-Tanzania ambapo watakuwa wakipima watu mbalimbali wenye matatizo ya macho BURE, wale wenye matatizo ya kutoona vizuri maandishi watapewa MIWANI za kusomea BURE.Jumla ya miwani zipatazo elfu kumi(10,000) zipo kwa ajili ya kugawiwa kwa watanzania ambao watabainika na matatizo hayo, Ratiba ya Clinic hiyo itakayokuwa na vituo vinne ni kama ifuatavyo.

Kituo 1:St Nicholaus Anglican Church –ILALA
Kituo cha 2:Tanzania Assemblies of GOD (TAG-Mbagala)
Kituo cha 3:Lutheran Chuch – Vingunguti
Kituo cha 4: Baptist Mission Church – Magomeni

Kliniki zote hizi zitakuwa zinaanza saa nne asubuhi mpaka saa kumi jioni

Donnie Moen kuhudumu

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...