29 January 2012

Rebecca - I Believe NEW SONG OF 2012

Rebecca releases her 4th single from her album titled 'I Believe" which is also the title of the Album. Video directed by multiple award winning director Uvi Orogun. Rebecca (Rebecca Jesus Conquer) has ministered across the world and seen many miracles take place.

CHECK THE VIDEO;

GOD RAISED ME WHEN I DIED IN A LONDON BUS..BY REBECCA!

Rebecca was Ms Africa (UK) 2000 and a club and events manager, organising fashion shows, beauty contests and gigs, during her events she will perform secular songs as part of the show. Rebecca also raised funds by organising events for various charities in West Africa.
                          Rebecca Jesus Conquer and   Sporah Njau;
Rebecca continued being a blessing to others with her singing in her church and other churches.
To satisfy the desire of both herself and her new fan base, she recorded her first gospel album called "FIRE 4 FIRE" in 2007. This album has strong attachments to her innermost feelings and emotions. Rebecca believes that through music she can express her emotions and love for the Lord and has devoted her career to gospel music.

In 2008 Rebecce released her second album "JESUS CONQUER" as a confirmation that the Lord has made her more than a conqueror. Her message is basic but powerful and well known for her warfare praise songs thats propels people to stand in spiritual warfare and battles. She hopes to influence the lives of our young men and women through her music in a positive way that will bring deliverance in their lives. Rebecca has dedicated her life and music to her Lord and saviour Jesus Christ as she ministers in and around United Kingdom and abroad;



Terrel FromTanzania, Rebecca From Sieraleon, Allen From Ghana and Sporah From The Sporah Show.

Mwimbaji wa nyimbo za injili Christina Shusho

Kwa muda mrefu sasa media nyingi za Tanzania zimekuwa zikiplay nyimbo za kundi la Christ Ambassadors Choir. Album ya kundi hilo kutoka Kigali Rwanda  iliyopewa jina la KWETU PAZURI (Video na Audio) kwa takribani miezi mitano  toka August 2011 imekuwa ikisikika sio tu kwenye media bali hata majumbani, mitaani na sehemu mbalimbali. Kitendo cha Christina shusho kuingiza sokoni album yake ya VIDEO iitwayo NIPE MACHO mnamo tarehe  tarehe 23/dec/2011 imeonekana kuteka hisia za wengi kwa utukufu wa Mungu.
Katika Video Album hiyo ya Shusho iliyofanywa tena na kampuni ya MBC HOTMEDIA, nyimbo ya kuabudu iitwayo NATAKA USHIRIKA NA WEWE ndiyo inayoongoza kuchezwa katika media mbalimbali ambapo tar 1jan 2011 nyimbo hiyo pamoja na Nyingine iitwayo NINA WIMBO zilichezwa kwa mara ya kwanza na katika kituo acha Television ya CITIZEN cha nchini Kenya katika kipindi cha RAUKA Kinachotayariswha na K-KREW.
Wakati Christina Shushu ameuanza Mwaka huu wa 2012 kwa kishindo kwa album yake hiyo ya Video, nguli mwingine wa Muziki wa injili nchini ROSE MUHANDO na yeye Mwaka huu wa 2012 anatarajia kuingiza sokoni album yake ya Video iitwayo” UTAMU WA YESU” baada ya ile ya Audio aliyoitoa mapema mwaka jana. Kufanya Vizuri kwa Video album hii ya NIPE MACHO ni hatua ya kwanza kabla hajaachia Video album yake nyingine iitwayo KWA KANISA LA KRISTO.




Viongozi wa Dini Nchini Uganda walalamikia Kitendo cha Mchungaji Kumwagiwa Tindikali
Viongozi wa Dini nchini Uganda wamelalamikia kitendo kilichofanywa na watu wasiojulikana cha Kumwagia Tindikali(Acid) usoni Mchungaji Umar Mulinde wa kanisa la GOSPEL LIFE CHURCH lililoko jijini kampala nchini humo.Kitendo hicho kilifanyika siku ya mkesha wa Christmas (Christmas Eve)  mara baada ya kumaliza kuongoza Ibada kanisani hapo.
Mch Umulinde alipata shambulio hilo majira ya saa tisa alfajiri baada ya mkesha kumalizika na baadaye aliwahishwa kupelekwa Hospitali na washirika wake katika International Hospital Kampala. Kwa Mujibu wa New Vision  Babaake na Pastor Umar alikuwa ni Imam na Mch Umar Mwenyewe alikuwa Sheikh kabla hajamkabidhi Yesu Maisha kama Bwana na Mwokozi wa Maisha Yake.

Baada ya Mch Umar kuokoka alipata vipingamizi vingi kutoka katika familia yake yenye msimamo mkali na dini ya Kiislamu. Shambulio hilo limepelekea Mchungaji Umar  kupoteza uwezo wa kuona wa jicho lake la kulia, huku upande wa kulia wa sura yake ukiwa umedhurika.

Akielezea tukio hilo akiwa hospitalini Mch Umar anasema baada ya kutoka kanisani kuna mtu mmoja alinifata akijifanya mkristo na kuniita kwa nguvu Pastor,  Pastor, Pastor, nilipogeuka kuangalia ninani anayeniita  ndipo aliponimwagia Tindikali usoni, nilipogeuka baada ya kumwagiwa mtu mwingine akanimwagia tena tindikali mgongoni kisha akakimbia akisema “Allah Akbar”( Mungu Mkubwa)”

Mch Umar amekuwa akiendesha mikutano ya Injili na kuwaambia watu wote hususani waislam wamgeukie kristo kama alivtofanya yeye. Kwa muda wote ambao yuko Hospitali Mch Amar amekuwa akiuguzwa na mkewe ambapo watumishi wengi nchini humo wamefika na kumuangalia pamoja na kufanya maombi.

Mchungaji Umar Mulinde kabla hajashambuliwa kwa Tindikali



Mchungaji Umar Mulinde akiwa katika moja ya mikutano yake akitangaza Habari njema za Ufalme wa Mungu

20 January 2012

LOWASSA AT NIGERIA CHURCH TB JOSHUA


BAADA ya kuandamwa na ‘kashikashi’ za kisiasa kwa muda mrefu, Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa (CCM), ameonekana ‘laivu’ runingani akifuatilia kwa karibu ibada ya Kiongozi Mkuu wa Huduma ya Kikristo ya Synagogue Church of All Nations (SCOAN), Mtume na Nabii Temitope Balogun Joshua ‘T.B Joshua’ huko Lagos, Nigeria.
Ishu hiyo ambayo imekuwa gumzo katika mitandao fulani fulani ilijiri hivi karibuni ambapo waziri mkuu huyo mstaafu alionekana kupitia Runinga ya Emmanuel TV.

Katika ibada hiyo iliyokuwa na ‘taito’ ya Sunday Live Service, ujumbe wa siku hiyo ulikuwa ni kushinda woga katika kujaribu kutenda jambo lolote.
T.B Joshua ni mmoja wa viongozi wenye heshima duniani aliyejipatia umaarufu kutokana na unabii anaoutoa kuhusu masuala mbalimbali, uponyaji kwa njia ya maombi na maombezi ya kawaida.

Sonnie Badu atoa Ushuhuda namna mtu alivyoponywa Kansa na Mwingine Utasa wakati akimuabudu Mungu


Sonnie Badu Ni Mwanamuziki wa Injili kutoka nchini Ghana Barani Afrika. Katika moja ya Ziara zake za kitumishi alitoa ushuhuda huu na kusema.

 “Jumapili  moja wakati  nikiuimba wimbo wa “Covenant Keeping God”  kanisani, ndani ya ibada hiyo  kulikuwa na Mwanamke aliyekuwa akitegemea kwenda kufanyiwa operation jumatatu (Kesho yake), mama huyo alikuwa akisumbuliwa na kansa ya titi. Mungu alisema na Mimi kuwa Muangalie huyo mwanamke na mpe Leso yako(kijitaulo cha kufutia uso-Face Towel).

Nilichokifanya nilimpa taulo ile naye akaiweka mahali palipokuwa na kansa. Wakati naendelea kuimba sikujua kuwa kuna uponyaji ulikuwa ukiendelea katika Mwili wa Mwanamke yule. Siku ya pili yake ndiyo ilikuwa appointment yake ya kufanyiwa operation.  Alipofika madaktari walipompima walimuuliza  nini kimetokea? hauna kansa tena, mpaka leo mwanamke Yule ni Mzima na hana kansa tena.

Mwanamke mwingine yeye alikuwa hajapata mtoto kwa Miaka Saba, wakati nauimba Wimbo huu Mungu alimponya Ugumba ,akaweza kushika Mimba na akapata mtoto, Our GOD is Covenant Keeping GOD”. Sonnie alisema Mungu wetu ni Mungu Mwenye kushika Maagano.

Sonnie Badu kwa Muda mrefu sasa amekuwa akimtumikia Mungu Barani ulaya. Tofauti na uimbaji Sonnie humtumikia Mungu kama mchungaji  na Kiongozi wa Huduma yake ya Sonnie Badu Ministries.Kwa sasa Sonnie ndiye Mwanamuziki bora wa Injili Barani Afrika  2010/2011 nafasi ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Ucheagu (Uche wa Double-Double) kwa miaka miwili mfululizo .


Facebook yamponza Flora Mbasha




Mwanamuziki maarufu wa injili Florah MbashaMTANDAO maarufu wa kijamii wa Facebook umemponza msanii mahiri wa muziki wa Injili nchini Tanzania, Flora Mbasha, baada ya mtu asiyefahamika ambaye ni shabiki wake kugandisha picha chafu za ngono kwenye ukurasa wake ambayo iliibuka mijadala na kushangaza wengi wiki iliyopita.

Mbasha aliyetamba na nyimbo kama 'Adui', 'Usife Moyo', 'Sauti ya Mnyonge' aliibuka kwenye mtandao huo na kutoa ufafanuzi.

"Bwana Yesu asifiwe wapendwa, naomba niwatake radhi kwa picha ambayo ilikuwa imetupiwa kwenye ukurasa wangu pia niwashukuru wote ambao mmenipigia simu kunieleza kinachoendelea kwenye Facebook yangu, pia nawashukuru wote mlionielekeza jinsi ya kuifuta maana nilijaribu nikashindwa.

"Lakini pia nimuombe anayetupia picha kama hizi kwenye ukurasa wangu aache upesi la sivyo nitaifunga mtu yeyote asitupie vitu vyake ingawa haikuwa nia yangu kwani hii ni kwa ajili ya Injili, watumishi wa Mungu kukutana kuzungumzia habari za Mungu na marafiki mbalimbali kuelimishana kuhusu Injili na mambo yote yenye maadili na sio jambo lisilompendeza Mungu.

"Kwa upande wangu nimekwazika sana kwani sikutegemea kama mtu mwenye akili timamu angefanya hivyo, ila nimemsamehe. Nia yangu ni nzuri sana, nataka watu tujadili mambo ya Mungu, tushauriane na hasa kutokana na huduma ya uimbaji niliyo nayo nahitaji sana ushauri wenu na mawazo.

"Pia niwashirikishe mambo mbalimbali kuhusu maisha yangu binafsi pamoja na huduma, ili kwa pamoja tuonyane na tusaidiane pamoja na kuombeana. Nawapenda sana wote na amani ya Yesu Kristo iwe nanyi."  CHANZO..GAZETI LA MWANASPOTI LA LEO 17 January 2012

11 January 2012

Wewe ni Bwana by Enid

Glorious Celebration

Glorious Celebration wakiwa katika mazoezi wakimsifu bwana. 


















Kongamano lilofanyika pale shule ya sekondari ya  FILBERT mwaka jana .Likipabwa na waimbaji wa nyimbo za injili GLORIOUS CELEBRATION





 Kutoka kushoto nimchungaji Anthon, Chase Msinga, Mwenyekiti wa Vijana Oscar Mnyirenda

Mimi mwenye nikiwa kiongozi wa   Glorious Celebration nikiimba na kumsifu bwana  siku ya Vijana Kibaha


                         Wanafunzi wa kibaa nao walikuwa wanamsifu mungu.



Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...